Connect with us

News

LSK yamtaka Inspakta Kanja kuweka wazi kifo cha Ojwang’

Published

on

Chama cha mawakili nchini LSK kinamtaka Inspakta jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja kuhakikisha kuna uwazi kufuatia kifo tatanishi cha mwanablogu Albert Ojwang’.

Akihutubia Wanahabari siku ya Jumatatu, rais wa LSK Faith Odhiambo alimwagiza Kanja kutangaza majina ya maafisa ambao wanazuiliwa wakiwemo wale waliomsafirisha Ojwang’ kutoka kaunti ya Homabay hadi jijini Nairobi.

Kanja alitangaza kuzuiliwa kwa maafisa polisi waliokuwa zamu katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi wakati Ojwang’ alipowasilishwa kituoni ambapo baadaye alipatikana akiwa na majeraha mabaya ndani ya seli.

Odhiambo aliongeza kuwa taarifa iliyotolewa na Inspakta Jenerali Douglas Kanja kuhusu kifo cha mwanablogu huyo haitosheleza kufafanua yaliyojiri.

“Kwa nini hajataja majini ya maafisa waliozuiliwa? Mbona anaficha? Wacha wakenya wafahamu. Tunataka kujua maafisa waliomchukuwa Ojwang’ je wao ni miongoni mwa wanaozuiliwa?”, alisema Odhiambo.

Rais huyo wa LSK pia alilaumu jinsi maafisa wa usalama walivyomshikilia Ojwang’ hadi akakutana na mauti yake

“Jinsi walivyomhudumia Albert Ojwang’ ni ukiukaji wa haki zake pamoja na wananchi wakenya. Hiki hakiwezi kuchukuliwa kama kisa cha kawaida kwa sababu kinaashiria namna mamlaka inavyohudumu ndani ya huduma ya maafisa wa polisi”, aliongeza rais wa LSK.

Wakati huo huo waanadamanaji pamoja na wanaharakati walikusanyika nje ya makafani ya City jijini Nairobi wakishinikiza hatua za haraka kuchukuliwa kuhusiana na kisa hicho.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending