News
Maandamano ya makumbusho ya Juni 25
Wakenya wa tabaka mbalimbali wamejitokeza katikati mwa miji mkuu nchini Kenya ikiwemo Nairobi, Mombasa, Nakuru, miongoni mwa miji mingine kuadhimisha makumbusho ya Juni 25.
Maandamano hayo ya kuwakumbuka vijana wa kizazi cha Gen z walioaga dunia kwenye maandamano ya kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2025 yanaendelea katikati mwa miji hiyo.
Katika jiji la Mombasa maandamano hayo yanaendelea kwa amani huku Wanaharakati wa kijamii na vijana wa Gen Z wakiandamana na maafisa wa polisi kwa njia ya amani na usalama wa hali ya juu.
Jijini Nairobi na Nakuru hali ni tofauti kwani waandamanaji hao walianza kurushia mawe na maafisa wa polisi kinyume na jinsi maandamano hayo yalivyotarajiwa huku maafisa wa polisi wakitumia vitoa machozi ili kuwatawanya waandamanaji.
Katika jiji la Nakuru hali ni sawa na Nairobi kwani mshikeshike wa maafisa wa polisi wa kukabiliana na ghasia na waandamanaji wanakabiliana vilivyo huku barabara zote na shughuli za kibiashara zikifungwa.
Katika jiji la Kisumu hali ni tofuati kwani hakuna maandamano anayoendelea katika jiji hilo huku shughuli za kawaida za kibiashara na uchukuzi zikiendelea kwa utaratibu.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

