Connect with us

News

Maelfu ya wakaazi wajitokeza kwenye matibabu ya bila malipo chuo kikuu cha pwani

Published

on

Wiki ya matibabu ya bila malipo ya mwaka 2025 inakamilika jumapili  ya tarehe 2, Novemba 2025, katika chuo kikuu cha Pwani kaunti ya kilifi, huku ikivutia maelfu ya wakaazi waliowasili kutafuta huduma za matibabu.

Wakaazi waliofika katika kambi hiyo ya matibabu walisema zoezi hilo linawapa fursa adimu ya kupata suluhu kwa matatizo yao ya kiafya, ambapo dawa za matibabu imekuwa changamoto kwa kuzifikia.

Wakaazi mmoja baada ya mwengine walieleza hisia zao kuhusiana na zoezi hili lililoasisiwa na wakfu wa wakili George Kithi, Chuo kikuu cha Pwani, COCOFM na wadau mbalimbali.

Akizungumza katika chuo kikuu cha pwani kunakoendelea zoezi hilo, mkurugenzi wa George Kithi Foundation, wakili George Kithi alisema wakaazi wa kaunti ya Kilifi wanauhitaji mkubwa wa huduma bora za afya.

Kithi alidokeza kuwa zoezi hilo litakuwa likifanywa mara kwa mara ili kuhakikisha wakaazi wa Kilifi na Pwani kwa jumla wanafikia huduma bora za afya, ili jamii iweze kuwa yenye afya inayostahili.

Wakili George Kithi akitembelea baadhi ya wagonjwa katika chuo kikuu cha pwani Kilifi.

Kwa upande wake mhadhiri wa chuo kikuu cha pwani profesa Halim Shauri, alipongeza uanzilishi wa mpango huo akidokeza kuwa chuo kikuu cha pwani kina mikakati ya kujenga hospitali kuu ambayo mbali na kutoa mafunzo ya kitaalamu, pia itasaidia kutoa huduma za afya kwa wakaazi wa pwani.

Baadhi ya wagonjwa waliofika katika chuo kikuu cha Pwani mjini Kilifi kupokea matibabu ya bila malipo.

Naye naibu msimamizi wa mpango wa kambi ya wiki ya matibabu ya bila malipo katika wakfu wa George Kithi daktari Julius Nyamawi, amesema zoezi hili limefaidi wakaazi wengi ambao wamekuwa na changamoto ya kupata matibabu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending