Connect with us

News

Mahakama ya Kilifi yamnyima dhamana mshukiwa wa ulaghai

Published

on

Kesi ya ulaghai wa shilingi milioni 1.2 inayomkabili mshukiwa Emmanuel Kithi imewasilishwa katika Mahakama ya Kilifi.

Mshukiwa Emmanuel Kithi anadaiwa kumlaghai mlalamishi Moses Mwafondo kwa kumuahidi kwamba atampea zabuni ya usambazaji wa bidhaa mbalimbali kwa Manuspaa ya Malindi zenye thamani ya shilingi 1,205,598.

Katika kesi hiyo iliyowasilishwa Mahakamani, mshukiwa Kithi inadaiwa kutekeleza kitendo hicho kati ya tarehe tofauti mnamo mwezi Disemba mwaka 2024 na mwaka 2025.

Hakamu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa alimnyima dhamana mshukiwa huyo pamoja na kuagiza kuzuiliwa rumande katika gereza la Kilifi, kaunti ya Kilifi.

Hakimu Obulutsa aliagiza mshukiwa kurejeshwa tena Mahakamani mnamo tarehe 25 mwezi Februari mwaka huu ambapo Mahakama itatoa uamuzi wa iwapo mshukiwa atapewa dhamana au la.

Hii ni baada ya upande wa ashtaka kupinga ombi lililowasilishwa na Wakili wa mshukiwa la kutaka Mahakama ilimuachilie kwa dhamana mteja wake baada ya kubainika kwamba ni mfanyikazi wa serikali ya kaunti ya Kilifi katika Idara ya jinsia, pamoja na kubainika kwamba amekuwa akitekeleza vitendo hivyo vya ulaghai kwa watu wengine.

Mshukiwa huyo hata hivyo alikanusha mashtaka dhidi yake, licha ya Mahakama kubaini kwamba jamaa huyo ana kesi nyingine ya kujibu ya shilingi milioni 1.6 katika Mahakama hiyo.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending