Connect with us

International News

Matumaini ya kusitisha vita Gaza yaanza

Published

on

Licha ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kwamba mpango wa usitishaji mapigano kwa siku 60 katika Ukanda wa Gaza unakaribia, kundi la Hamas limeeleza kwamba bado mazungumzo yanaendelea.

Katika kile kinachoonekana kama jibu la kwanza la Hamas tangu Rais Trump kutangaza kupatikana kwa mwafaka huo, kundi hilo lilisema kwamba bado linaendelea kuyatafakari mapendekezo mapya yaliyomo kwenye mpango huo.

“Tunalichukulia suala hili kwa uangalifu mkubwa. Tunafanya majadiliano ya kitaifa kuyatathmini mapendekezo ya ndugu zetu wapatanishi”, lilisema kundi hilo kupitia Kiongozi wao.

Mnamo siku ya Jumanne Julai mosi mwaka huu, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Israel ilikuwa imekubaliana na masharti ya kusitisha mapigano kwa siku 60 wakati mauaji kwenye ukanda wa Gaza yakiwa kwenye mwezi wake wa 21.

Trump alidai kwamba Misri na Qatar, ambazo ni wapatanishi wakuu, walikabidhiwa jukumu la kuwafikishia mapendekezo hayo Hamas lakini wakati huo huo akilitishia kundi hilo kutokuutakaa mpango huo.

“Tunaamini kwamba Misri na Qatar wanaendelea na mpango mzuri wa upatanisho na suala hili linafaa kuchukuliwa kwa uzito zaidi lakini pia ni lazma Hamas iwe waangalifu na kuzingatia masharti hayo”, alisema Trump.

Baraza la usalama lajadili upatishi Gaza.

Waziri wa Mambo ya nje wa Israel, Gideon Saar, alisema sehemu kubwa ya mawaziri kwenye serikali ya nchi yake wanaunga mkono makubaliano hayo ambayo yanajumuisha kuachiliwa kwa mateka.

Waziri huyo wa mambo ya kigeni aliongeza kwamba sehemu kubwa ya raia wa Israel wanaunga mkono makubaliano hayo kama inavyothibitishwa na uchunguzi wa maoni.

Hata hivyo, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anatarajiwa kukutana na Rais Trump wiki ijayo mjini Washington, ili kuangazia zaidi mikakati na mipango ya kudhibiti.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Vita dhidi ya Al-Shabab vya shika kasi Somalia

Published

on

By

Operesheni kali ya kijeshi inayoendelea nchini Somalia ambapo zaidi ya wanamgambo 33 wa kundi la Alshabab wameuawa katika eneo la Shabelle nyanda za chini za Jubaland.

Ufanisi wa operasheni hii ya hivi punde ni muendelezo wa oparesheni iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Aprili 24 katika eneo hilo la Juba ambapo Wanamgambo 27 wa AlShabab waliuawa.

Hii ina maana kwamba Jeshi la Somali limefanikiwa kuvunja maficho muhimu ya kundi hilo, ambalo kufikia sasa ya Wanamgambo 60 wameuawa

Kwa mujibu wa vianzo vya habari hususan kutoka kwa maafisa wa usalama, operesheni hiyo inafanyika kufuatia taarifa za kijasusi kuhusu maficho ya wanamgambo hao waliokuwa wakipanga mashambulizi dhidi ya vituo muhimu na taasisi za serikali.

Wanajeshi hao walivamia ngome za magaidi hao kwa ustadi mkubwa, wakifanikiwa kudhibiti eneo hilo baada ya mapambano makali yaliyochukua muda wa saa kadhaa.

Maafisa wamesema kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuimarisha usalama na kuangamiza kabisa mtandao wa Al-Shabaab ambao kwa muda mrefu umekuwa ukihatarisha amani katika maeneo mbalimbali ya Somalia na ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Wananchi wa eneo la Jubbaland wameelezea matumaini mapya kufuatia operesheni hiyo, wakisema kuwa hatua hiyo inaleta nuru ya kurejea kwa utulivu na maendeleo baada ya miaka ya hofu na mashambulizi ya mara kwa mara nchini.

Serikali imeapa kuendeleza msako dhidi ya wanamgambo hao hadi pale watakapokomesha kabisa vitisho vya mashambulio , huku ikiwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kudhibiti ugaidi.

Taarifa ya Billy Mongo

Continue Reading

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending