Connect with us

International News

Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni

Published

on

Mahakama kuu nchini Tanzania imemrejesha kwenye debe mgombea urais wa chama cha upinzani ACT wazalendo, Luhaga Mpina na kupindua maamuzi yaliyotolewa na tume ya uchaguzi nchini humo INEC.

Hii inamaana tume ya INEC ni lazima imjumuishe Mpina katika orodha ya majina ya watakaopigiwa kura, hatua itakayosababisha upinzani kwenye uchaguzi huo mkuu.

Hatua hii sasa inampa Mpina fursa ya kuanzisha kampeni za kutaka kumbandua mamlakani rais Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 29 mwaka 2025.

Kampeni za uchaguzi tayari zinaendelea nchini humo.

INEC ilimzuia mpina kugombe wadhifa wa urais mwezi Agosti 26, 2025 ikidai chama cha ACT Wazalendo kilikiuka taratibu za chama kwa kumsimamisha Mpina kuwania wadhifa huo.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa katika kampeni za uchaguzi mkuu.

Katika uamuzi uliotolewa Alhamisi  mwezi Septemba 11, 2025, jopo la majaji watatu mjini Dodoma liliagiza INEC kumuidhinisha Mpina kama mgombea wa urais.

Anatarajiwa kujumuika na wagombea wengine 16 kutoka vyama vidogo vya kisiasa katika mapambano hayo ya kuwania urais, ambao wote wanania ya kung’atua rais wa sasa Samia Suluhu Hassan mamlakani.

Chama cha Chadema kilizuiwa kugombea katika uchaguzi huo baada ya kiongozi wake Tundu Lissu kufunguliwa mashtaka ya uhaini.

Kiongozi wa upinzani wa Chadema Tundu Lissu akiwa mahakamani.

Rais Samia Suluhu Hassan alichukua hatamu za uongozi kama rais baada ya kifo cha John Pombe Magufuli mwaka 2021.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

International News

Rais wa Cameroon amteua mwanawe kuwa makamu wa rais

Published

on

By

Taifa la Cameroon limeidhinisha mabadiliko ya kisheria kuhusu wadhfa wa makamu wa rais na kumpa mamlaka zaidi rais wa taifa hilo kufanya uteuzi upya.

Sheria hiyo mpya, inampa uwezi makamu wa rais kuchukua nafasi ya rais moja kwa moja iwapo rais wa taifa hilo amefariki ama amekubwa na ugonjwa na kushindwa kuendelelea na majukumu yake kama rais kabla ya uchaguzi kuandaliwa.

Bunge la taifa hilo siku ya Jumamosi liliidhinisha mabadiliko hayo ya kisheria na kutoa nafasi ya kuteuliwa kwa makamu wa rais ili kuhakikisha shughuli za kiserikali zinaendeshwa vyema baada ya bunge la kitaifa na seneti kupiga kura na kufanya mabadiliko hayo ya kisheria katika taifa hilo la Cameroon.

Wabunge wa bunge la kitaifa na Seneti nchini Cameroon walipiga kura 200 huku wengine 18 wakipinga na wengine 4 wakikwepa kikao hicho cha bunge, hatua iliyopelekea mswada huo kupitishwa.

Hatua hiyo sasa imefanya Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 kumteua mwanawe Franck Emmanuel Biya kuwa makamu wa kwanza wa rais katika taifa hilo.

Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 na mwanawe Franck Emmanuel aliyemteua kuwa makamu wa rais wa taifa hilo.

Ni hatua ambayo imeibua mjadala mkali nchini Cameroon na bara Afrika kwa jumla baada ya uteuzi huo kutangazwa rasmi Aprili 4, 2026.

Sheria hiyo pia imepiga marufuku wananchi wa taifa hilo kujadili kuhusu hali ya afya ya rais Biya, kukosoa utendakazi wake pamoja na maamuzi yanayofanywa na Ikulu ya rais.

Emmanuel amehudumu katika wadhfa wa mkuu wa majeshi mbali na kushikilia cheo kikuu katika wizara ya ulinzi nchini humo.

Rais Biya amekuwa mamlakani tangu 1982 na alishinda muhula wa nane kwenye uchaguzi mkuu mwaka uliopita.

Kuidhinishwa kwa mabadiliko haya ya kisheria nchini Cameroon kunatambulika kama tukio la kihistoria tangu mwaka 2008 ambapo taifa hilo lilishuhudia pingamizi za kisheria kutoka kwa wananchi baada ya bunge la kitaifa kuongeza hatamu ya uongozi wa rais na kusababisha maandamano makubwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending