News
Mihadarati ya thamani ya Ksh. 2.19M imenaswa Mombasa
Maafisa wa kitengo cha kupambana na dawa za kulevya mjini Mombasa wamefanikiwa kuwakamata washukiwa wawili wanaodaiwa kuhusika na usambazaji wa mihadarati yenye thamani ya shilingi milioni 2.1.
Washukiwa hao, Mwanaisha Abdalla Gona mwenye umri wa miaka 42 na Nancy Njeri mwenye umri wa miaka 37, walikamatwa katika operesheni ya pamoja katika eneo la Kwa Hola huko Changamwe kaunti ya Mombasa.
Maafisa wa DCI wamesema operesheni hiyo ilifanikishwa baada ya kupokea taarifa za kijasusi ambapo polisi walipata misokoto 902 ya bangi iliyokuwa tayari kuuzwa, na gramu 300 za Heroini, huku thamani ya dawa hizo ikikadiriwa kuwa shilingi milioni 2.19.
Vifaa vingine vilivyopatikana ni pamoja na mizani ya kidijitali na mifuko ya plastiki ya kufungia dawa hizo, hali inayodokeza kuwa washukiwa hao walikuwa wakihusika katika mtandao wa usambazaji wa Mihadarati.
Washukiwa hao wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha Chaani, wakisubiri kufikishwa Mahakamani huku maafisa wa DCI wakisema wataendelea kuwasaka wahusika wa biashara ya dawa za kulevya ili kukomesha mtandao huo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

