Connect with us

News

Miili mingine 4 yapatikana kwa Binzaro- Shakahola

Published

on

Mili mingine minne imepatikana ikiwa imeoza kiasi cha kutotambulika katika msitu wa Shakahola karibu na kijiji cha Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Mili hiyo ilipatikama na wenyeji waliokuwa wakiendelea na shughuli zao katika msitu huo ambao umegonga vichwa vya habari tangu sakata ya Mhubiri tata Paul Mackenzie.

Kupatikana kwa miili hiyo ilisababisha idadi ya maiti zilizopatikana katika kisha cha hivi punde kabisa cha mauaji kwenye kijiji cha Binzaro kufikia Miili minane.

Maafisa wa usalama wanatarajiwa kukusanya mabaki ya hayo ili kuyapeleka katika makafani ya hospitali ya Malindi ambako
miili mingine iliyopatiakana katika kisa cha kwanza cha mauaji ya Shakahola ‘One’ inahifadhiwa.

Majuma mawili yaliyopita, Maafisa wa Polisi walivamia msitu huo na kupata maiti nne na makaburi sita ambayo sasa yanasubiri kufukuliwa.

Wahusika waliokuwa wakiendesha mafunzo ya itikadi kali katika eneo hilo lenye vijumba vitamo, waliwahi kutoroka wakiacha maiti moja ambayo ilikuwa haijazikwa.

Shughuli za kufukua makaburi hayo bado haijafanyika huku eneo hilo la msitu wa Kwa Binzaro likiwekwa chini ya ulinzi wa maafisa wa usalama.

Msako dhidi ya maafisa hao bado unaendelea katika msitu huo wa Shakahola.

Mackenzie na wenzake 30 walikamatwa na sasa wanasubiri kukamilika kwa kesi yake inayoendeshwa katika Mahakama za mjini Mombasa.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending