News
Misitu ya Kaya Hatarini
Mwenyekiti wa Shirika la Malindi District Cultural Association, MADCA Stanley Kahindi Kiraga amesema misitu ya Kaya iko katika hatari ya kuangamizwa licha ya kuwa misitu hiyo ni muhimu kwa jamii.
Kiraga alisema misitu hiyo ni mojawapo ya vyombo vinavyotumika kuhifadhi turathi na mila za jamii ya Mijikenda kwenye kaunti za Kilifi na Kwale.
Akizungumzia mpango wa kutumika kwa takriban ekari tatu katika kufanikisha mradi wa maendeleo kwenye msitu wa Kaya fungo katika kaunti ya Kilifi, Kiraga alipinga vikali mpango huo.
Kwa upande wake Afisa wa Shirika la kutetea haki za kibinadamu la Tema Digital Research Trust, Eric Mgoja alikashifu kuingiliwa kwa misitu ya Kaya akisema ni ukiukaji mkubwa wa mila na desturi za kijamii ikizingatiwa kwamba misitu hiyo ni ya kiasili.
“Ni wakati sasa wa wazee wa kaya na wanajamii wa Mijikenda kushirikiana ili kuhakikisha kuwa ardhi za misitu ya kaya zinasajiliwa kisheria”, alisema Mgoja.
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa Shirika la utetezi wa haki za ardhi nchini Kenya Land Alliance, Faith Alubbe alisema suala hilo litasaidia katika kulinda na kuhifadhi misitu ya Kaya dhidi ya wanyakuzi.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

