Sports
MTG United Wana Malengo ya Kucheza Ligi Kuu
Mkufunzi wa kilabu ya akina Dada ya Moving The Goal Post marufu kama MTG United kaunti hii ya Kilifi Fadhili Hamisi marufu coach Tibo amesema kwamba wanalenga kushiriki ligi ya FKFWPL siku za usoni.
Kwenye mahojiano ya kipekee na Kipenga Cha CoCo FM mwalimu huyo ana imani wa kikosi Bora kutimiza malengo hayo. “Nataka MTG United iwe timu ya kwanza ya akina Dada kaunti ya Kilifi kushiriki ligi ya akina Dada nchini kwani Wana uwezo huo.
“Aidha mwalimu huyo amesema licha ya changamoto chungu nzima wanazokumbana za kifedha Lengo lao si kuona tu timu hiyo inapaa Bali pia kuona badhi ya akina Dada hao wanacheza ligi za ndaani na nje za nchi siku za usoni. “Ni wasichana ambao Wana Vipaji itafurahisha sana wakicheza ligi ya ndaani na nje ya nchi hii siku za badaye.
“Vilevile mwalimu huyo ameongezea licha ya Soka akina Dada hao wanapewa mafunzo mengine ikiwemo jinsi ya kuishi vizuri katika jamii,msongo wa mawazo miongoni mwa mengine.
“MTG United haideal tu na soka tuko na vitengo vingine vya kuisaidia makuzi ya mtoto wa kike kama kujitambua katika jamii wanapoingia wakiwa wachanga kuanzia umri wa miaka 9-25.
” MTG United yenye makao hapa mnarani iko nafasi ya Saba ligi ya Supa baada ya kushiriki mechi 15.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

