News
Mung’aro achaguliwa kuwa Mwenyekiti wa ODM kaunti ya Kilifi
Uchaguzi wa viongozi wa mashinani wa Chama cha ODM katika kaunti ya Kilifi ulifanyika Agosti 25, 2025 licha ya awali kuhushudiwa vurugu baada ya kutofautiana kwa wafausi wa chama hicho.
Gavana wa kaunt ya Kilifi Gedion Mung’aro alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi na kuchakuwa nafasi ya Teddy Mwambire, baada ya kumbaduliwa uongozini kama Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi.
Naibu Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi alichaguliwa Joseph Chilumo, Katibu mkuu akichaguliwa Ken Chonga ambaye ni mbunge wa Kilifi Kusini na Mwekahazina akachaguliwa Paul Katana ambaye ni Mbunge wa Kaloleni katika uchaguzi huo wa viongozi wa mashinani wa chama cha ODM katika kaunti ya Kilifi.
Mengine waliochaguliwa ni pamoja na Tima Abuu, Abdallah Kombe, Caro Kalume, Mae Mwadena, Nickson Muramba, Harrison Kombe Twahir Abdul, Rashid Mohamed miongoni mwa viongozi wengine.
Vurugu hizo zilitokea wakati wasimamizi kwenye lango la ukumbi huo wanaoegemea mrengo wa Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro, walipodai kwamba baadhi ya wanachama sio wanachama halisi.
Wafuasi wa Mwakilishi wadi ya Ganda Oscar Wanje ambaye alikuwa anawania wadhifa wa uenyekiti wa vijana kaunti ya Kilifi alilazimika kujiondoa katika wadhfa huo kwani ni kati ya miongoni mwa wale waliozuiliwa kuingia katika ukumbi wa uchaguzi huo na nafasi hiyo ikachaguliwa Abdallah Kombe.
Wafuasi hao walikosoa utaratibu mzima wa maandalizi ya uchaguzi huo, wakishikilia kwamba watawasilisha malalamishi yao kwa kamati kuu ya uchaguzi ya chama cha ODM kupinga uchaguzi huo.
Wafuasi hao wakiongozwa na Mwakilishi wadi ya Ganze Karisa Ngirani, walilaumu utaratibu wa shughuli hiyo, wakisema umekosa kuzingatia haki ya wanachama.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni
Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali
Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.
Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.
Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.
Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.
Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.
Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke
Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.
Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.
Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.
Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.
Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.
Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.
Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

