News
Mung’aro: Miradi yote ya kaunti kukamilika 2026
Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amesema serikali yake iko mbioni kuhakikisha miradi yote ya maendeleo katika kaunti inakamilika kufikia mwezi juni mwaka ujao wa 2026.
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi hundi kwa makundi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo wanaoishi na ulemavu na wakongwe mjini Kilifi, gGavana Mung’aro alisema miongoni mwa miradi hiyo ni ufunguzi wa uwanja mpya wa michezo mjini Kilifi, uzinduzi wa makao makuu ya kaunti miongoni mwa miradi mingine.
Gavana Mung’aro pia alidokeza kuwa serikali yake inapanga kuanzisha ujenzi wa hospitali ya Ganze ambao utagharimu zaidi ya shilingi milioni 350.
Kiongozi huyo wa kaunti alisema ujenzi wa makao makuu ya kaunti unaendelea na utakapokamilika utarahisisha upatikanaji wa hudumua kwa wakaazi wa Kilifi vile vile kupunguza gharama ya matumizi ya fedha kwa kaunti.
“Kila mradi ambao tumeanza lazima ukamilike kufikia juni 2026, lazima tufungue makao makuu ya kaunti, lazima tufungue kiwanja chetu kipya cha mpira, lazima tufungue hospitali zetu za Mariakani, Kilifi, Bamba, pia tutaanza kujenga hospitali ya Ganze ya zaidi ya shilingi milioni 350”, alisema Mung’aro.
Wakati huo huo alishauri makundi yaliyopokezwa hundi hizo kuhakikisha wanazitumia kuekeza kwenye miradi ya maendeleo ili kuboresha maisha yao vile vile kunufaisha makundi mengine.
“Haya ndiyo mabadiliko tunayoyakusudia tulipoanzisha mfuko wa wezesha, hata hivyo uendelevu wa mfuko huu unategemea ulipaji wa mikopo kwa wakati, kila malipo yanaporejeshwa yanatuwezesha kufadhili makundi mengine yaliyotuma maombi, leo hii tunapozindua rasmi mpango huu wa uzima cash transfer ambao unalenga jamii zetu zisizojiweza hasa wazee katika wadi zote 35, tuko na watu 1,205 kila mmoja atapata shilingi 18,000 ambazo ni malimbikizi ya miezi tisa iliyopita.
Taarifa ya Joseph Jira.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

