Connect with us

News

Mung’aro: Miradi yote ya kaunti kukamilika 2026

Published

on

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amesema serikali yake iko mbioni kuhakikisha miradi yote ya maendeleo katika kaunti inakamilika kufikia mwezi juni mwaka ujao wa 2026.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi hundi kwa makundi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo wanaoishi na ulemavu na wakongwe mjini Kilifi, gGavana Mung’aro alisema miongoni mwa miradi hiyo ni ufunguzi wa uwanja mpya wa michezo mjini Kilifi, uzinduzi wa makao makuu ya kaunti miongoni mwa miradi mingine.

Gavana Mung’aro pia alidokeza kuwa serikali yake inapanga kuanzisha ujenzi wa hospitali ya Ganze ambao utagharimu zaidi ya shilingi milioni 350.

Kiongozi huyo wa kaunti alisema ujenzi wa makao makuu ya kaunti unaendelea na utakapokamilika utarahisisha upatikanaji wa hudumua kwa wakaazi wa Kilifi vile vile kupunguza gharama ya matumizi ya fedha kwa kaunti.

“Kila mradi ambao tumeanza lazima ukamilike kufikia juni 2026, lazima tufungue makao makuu ya kaunti, lazima tufungue kiwanja chetu kipya cha mpira, lazima tufungue hospitali zetu za Mariakani, Kilifi, Bamba, pia tutaanza kujenga hospitali ya Ganze ya zaidi ya shilingi milioni 350”, alisema Mung’aro.

Wakati huo huo alishauri makundi yaliyopokezwa hundi hizo kuhakikisha wanazitumia kuekeza kwenye miradi ya maendeleo ili kuboresha maisha yao vile vile kunufaisha makundi mengine.

“Haya ndiyo mabadiliko tunayoyakusudia tulipoanzisha mfuko wa wezesha, hata hivyo uendelevu wa mfuko huu unategemea ulipaji wa mikopo kwa wakati, kila malipo yanaporejeshwa yanatuwezesha kufadhili makundi mengine yaliyotuma maombi, leo hii tunapozindua rasmi mpango huu wa uzima cash transfer ambao unalenga jamii zetu zisizojiweza hasa wazee katika wadi zote 35, tuko na watu 1,205 kila mmoja atapata shilingi 18,000 ambazo ni malimbikizi ya miezi tisa iliyopita.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending