Connect with us

News

Mwalimu wa Madrasa adaiwa kumlawiti mvulana eneo la Kwa Mwango mjini Kilifi

Published

on

Hali ya wasiwasi na ghasia zilishuhudiwa katika eneo la Kwa Mwango karibu na Mkoroshoni mjini Kilifi Agosti 28, 2025.

Hii ni baada ya wakaazi wenye hasira kuvamia madrassa ya msikiti wa Masjid Rehema, wakipinga tuhuma za udhalilishaji wa watoto unaofanywa na Mwalimu wa Madrasa hiyo.

Kulingana na walioshuhudia tukio hilo walisema kisa hicho kilidhiirika wakati mama mmoja alipofichua kwamba mwanawe ambaye ni mwanafunzi wa madrasa hiyo kwamba alilawitiwa na mwalimu mmoja wa madrasa hiyo.

Mama huyo ambaye alikuwa akipiga nduru na kulalamikia madhila aliyofanyiwa mwanawe yalisababisha umati wa watu kuvamia madrassa hiyo na bweni la wanafunzi hao, wakitaka kuchoma majengo ya madrassa hiyo kwenye msikiti huyo wa Masjid Rehema.

Wakaazi hao walivamia msikiti huo wakiwa na dhamira ya kumuadhibu Mhubiri huyo huku wengine wakifunga barabara ya Kilifi – Malindi pamoja na kuwasha moto, hali iliyosababisha msingamano wa magari katika eneo hilo ambalo kwa kawaida huwa na shughuli nyingi.

Wenyeji hao walivunja lango na kuingia msikitini na kuanza kumshanbulia Mhubiri huyo ambaya baadaye aliokolewa na Maafisa wa usalama ambao walimkamata mshukiwa na kumpeleka kituo cha Polisi mjini Kilifi.

Maafisa wa Polisi wamnusuru Mwalimu wa madrassa ya msikiti wa Masjid Rehema

Maafisa hao wa usalama wameeleza vyanzo vya habari Kwamba wanaendelea na Uchunguzi na mshukiwa atafikishwa mahakani hivi karibuni.

Taarofa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending