News
Mwanaume wa umri wa makamu ahukumiwa kifungo cha miaka 7 gerezeni
Mahakama ya Kilifi imemhukumu kifungo cha miaka 7 gerezani mwanaume mmoja aliyepatikana na hatia kwa kesi ya biashara ya meno za ndovu baada ya uchunguzi na ushahidi kukamilika.
Akitoa hukumu hiyo, Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa alisema kuwa mshtakiwa Abdallah Mbithi ana siku 14 kisheria za kukata rufaa endapo hajaridhishwa na hukumu hiyo.
Hukumu hiyo ilitolewa baada ya uamuzi wa Mahakama kubaini kwamba Mbithi alipatikana na hatia baada ya Mahakama kuzingatia ushahidi uliotolewa ikiwemo ushahidi wa mshtakiwa wa kujitetea.
Hakimu Obulutsa aidha alisema kuwa ndovu wako katika hatari kubwa ya kuuwawa hivyo basi kesi hiyo inayohusisha wanyamapori ina hukumu kali yenye kifungo cha maisha au kutoa faini ya shilingi milioni 20 hivyo mahakama imezingatia malilio yake na kumpuguzia kifungo hicho cha miaka saba.
Awali Mahakama ilielezwa kwamba mshtakiwa alipatikana na kipande cha sehemu ya ndovu iliyoshukiwa kuwa pembe ya ndovu ambapo baadaye daktari aliyefanya uchunguzi wa maabara alithibitishia mahakama kwamba kipande hicho ni sehemu ya jino la ndovu na uzani wake ni kilo 3 yenye thamani ya shilingi laki 3.
Taarifa ya Teclar Yeri.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

