News
Mbinu mpya ya kuwaua wakongwe Kilifi na Kwale yaibua hofu
Mashirika ya kutetea haki za binadamu eneo la pwani yameeleza wasi wasi wao kuhusu madai ya kuibuka kwa mbinu mpya ya mauaji ya wazee katika kaunti ya Kilifi na Kwale kutokana na mizozo ya umiliki wa ardhi.
Kwa mujibu wa afisa wa shirika la Haki Yetu John Obonyo, kwa sasa wahusika wanatumia mbinu ya kuteketeza moto nyumba za wazee sawa na kuwanyonga ili kuonekana wamejitoa uhai ili kupoteza ushahidi.
Obonyo hata hivyo alibaini kwamba watu hulipwa kati ya shilingi elfu tatu hadi shilingi elfu nne, ili kutekeleza mauaji hayo.
“Mauaji ya wazee yamezidi sana, yamezidi kwa misingi kwamba mbinu ambayo wazee wanapoteza uhai imebadilika, njia moja ni kuwa wanachomwa kwa nyumba kusudi wapoteze ushahidi, njia ya pili ni kuwa wananyongwa, na mtu ambaye amejinyonga nitofauti na yule ambaye amenyongwa, kwa hivyo ni njia tu yakupoteza ushahidi, lakini cha kusikitisha zaidi ni kuwa imekuwa na bei, sehemu za kilifi ukiwa na elfu 30 unatoa uhai”,alibaini Obonyo.
Hata hivyo Obonyo alipendekeza wazazi kuandika wosia kwa familia zao wakati wa uhai wao ili kuepuka mizozo kama hiyo kushuhudiwa.
Kaunti za Kilifi na Kwale zimekuwa zikiongoza kwa visa hivyo ambapo wakongwe wamekuwa wakiuawa kwa tuhuma za ushirikina, japo ilibainika kuwa mauaji hayo yanachangiwa na wanafamilia kutaka kurithi mali.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

