Connect with us

News

Odinga, anataka fedha za NG-CDF kusambazwa kwa kaunti

Published

on

Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga amependekeza fedha zote zinazosambaza kwa hazina ya NG-CDF na NGAAF, kufanywe marekebisho ili fedha hizo kusambazwa kwa serikali za kaunti.

Odinga alisema kila kitu ambacho wakenya wamefanya ni kurudisha utawala bora, na wamefanya hazina ya NG-CDF kuwa ya kizamani na kwamba fedha hizo zinafaa kutumwa kwa serikali za kaunti kwani hazina hiyo hatambuliki kikatiba.

Akihutubia Kongamano la Ugatuzi katika kaunti ya Homabay, Odinga alishikilia msimamo wake kwamba ni lazima ugatuzi upewe kipau mbele na masuala yote yaliyogatuliwa kusimamiwa na serikali za kaunti. 

“Hazina ya NG-CDF na NGAAF zinapokea fedha nyingi na kutumika kwa mambo ya basari, hii pesa inafaa kutumwa kwa serikali za ugatuzi kwani hazina ya NG-CDF ilipitwa na wakati na hatambuliki kikatiba na iwapo kutafunywa marekebisho basi pesa hizo zitasaidia ugatuzi kuimarika zaidi”, alisema Odinga.

Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga katika Kongamano la ugatuzi, Homabay{Picha kwa hisani}

Wakati huo huo amevisuta vyombo vya habari, akisema baadhi ya vyombo vya habari nchini vimekuwa vikilipwa ili kufichua sakata za ufisadi nchini, akisema ni lazima kila mmoja achukue jukumu la kupambana na ufisadi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending