Connect with us

News

Odinga, awasuta wapinzani dhidi ya kauli ya Wantam

Published

on

Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga ameonekana kuunga mkono ushirikiano kati ya chama cha UDA na ODM, na akawasuta wapinzani dhidi ya kauli yao ya Wantam.

Odinga aliwataka wakenya na upinzani kuipa nafasi serikali kukamilisha ajenda yake na kisha wananchi watafanya uamuzi wao ifikapo uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027. 

Akizungumza wakati wa mazishi ya Pheobe Asiyo katika kaunti ya Homabay, Odinga aliweka wazi kwamba juma lijalo kutakuwa na mkutano wa Muungano wa wabunge ambao utaangazia masuala mbalimbali muhimu. 

“Niko na imani kwamba masuala mbalimbali anayoihusu taifa yatatekelezwa na tunaomba mtupe nafasi kisha ikifika uchaguzi mkuu mwaka 2027 wakenya ndio wataambua sio tu kubweka bweka na Wantam wantam”, alisema Odinga.

Wakati huo huo aliitaka serikali kufanikisha mchakato wa fidia kwa wananchi ambao wamepoteza maisha yao wakati wa maandamano ya ghasia, akisisitiza suala kangazia majanga ya maandamano ya mwaka wa 2017. 

Kauli za viongozi hao zimejiri baada ya kuafikiwa mpango wa kufanikisha ajenda 10 kwenye mkataba wa ushirikiano wa kitaifa kati ya chama cha UDA na ODM pamoja na kuidhinishwa kwa ripoti ya NADCO.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending