Connect with us

News

Ofisi ya ODPP kufungua mashtaka ya mauaji dhidi ya Masinde

Published

on

Mkurugenzi wa mashtaka ya umma, Renson Ingonga, ameidhinisha mashtaka ya mauaji dhidi ya afisa wa polisi Barasa Masinde.

Masinde anadaiwa kuhusika moja kwa moja na mauaji ya mchuuzi wa barakoa Boniface Kariuki aliyepigwa risasi katikati mwa jiji la Nairobi wakati wa maandamano ya kupinga mauaji ya Albert Ojwang.

Kwenye taarifa iliyotolewa Julai 10, 2025, Ingonga alisema ushahidi uliokusanywa unatosha kufungua kesi ya mauaji dhidi ya afisa huyo wa Polisi, akisisitiza kwamba ni lazima haki ipatikane kwa familia ya marehemu Boniface.

Afisa mwingine aliyekuwa anachunguzwa kwa kuhusika na tukio hilo, Duncan Kiprono, aliondolewa lawama na kuachiliwa huru kwa kukosa ushahidi wa moja kwa moja dhidi yake.

Familia ya marehemu Boniface pamoja na Wanaharakati wa haki za binadamu wamekuwa wakishinikiza haki itendeke, wakitaka wote waliohusika na mauaji ya Boniface wakabiliwe kisheria.

Afisa Masinde anatarajiwa kufikishwa Mahakamani siku zijazo kujibu mashtaka yanayomkabili, huku serikali ikishikilia kwamba maafisa wa polisi wanaokiuka majukumu yao ya kikazi ni lazima wawajibishwe.

Itakumbukwa kwamba Juni 17 mwaka huu wakati wa maandamano ya kupinga mauaji ya Mwanablogu na Mwalimu Albert Ojwang, vurugu zilishuhudiwa katikati mwa jiji la Nairobi na kusababisha baadhi ya vijana wa Gen Z kupoteza maisha yao akiwemo Boniface Kariuki.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending