News
Panda shuka za kiuongozi katika serikali za ugatuzi
Huku Kongamano la Ugatuzi awamu ya 12 likiendelea kaunti ya Homa Bay, bado Wakenya wanaendelea kutathmini iwapo malengo ya ugatuzi yanatimizwa.
Yapo maswali mengi tu kuhusu ufanisi wa kimaendeleo na utenda kazi wa serikali za kaunti ambazo hadi sasa nyingi zao zinazidi kulaumiwa kwa kuendeleza ufisadi, usimamizi mbaya wa rasilimali, na utoaji wa huduma duni, suala ambalo limeendelea kuwamulika magavana na maafisa wengine wa serikali za kaunti.
Tangu Ugatuzi uanzishwe baada ya katiba mpya ya mwaka 2010, Bunge la seneti limetenga takribani shilingi trillioni 4 kwa serikali za ugatuzi kupitia mfumo wa ugavi wa rasilimali za serikali kwa huduma za kaunti, ingawa bado kuna maswali mengi kuliko majibu kuhusu malengo yaliyokusudiwa sheria hii ya ugatuzi.
Uongozi wa serikali hizi bado upo kwenye mizani na mitihani mingi tu, ikiwa ni pamoja na ahadi nyingi zinazotolewa na viongozi wa serikali hizi za kaunti ambazo hazitimizwi kutokana na kile wananchi wanadai ni ukiritimba unaotokana na uongozi mbaya, ufisadi na upendeleo katika utoaji wa huduma na kandarasi.
Suala la utoaji wa kandarasi limekuwa donda sugu katika serikali nyingi za kaunti, huku zikiendelea kukabiliwa na malimbikizi ya madeni.
Miongoni mwa sekta zinazotajwa kuathirika zaidi na usimamizi mbaya au ufujaji wa pesa za umma ni sekta ya afya ambayo. Hospitali nyingi hazina dawa huku huduma za afya zikiendelea kudorora kuanzia ngazi za zahanati hadi hospitali kubwa za kaunti.
Serikali za kaunti pia zinashtumiwa kwa kuendelea na uratibu wa miradi hewa katika bajeti zao, na kupelekea kupotea kwa mabilioni ya pesa za uma.
Japo Ugatuzi ulilenga kuboresha maisha ya Wananchi katika ngazi za chini, bado umaskini umekithiri huku mizozo ya uongozi na utawala wa kibepari vikiendelea kushuhudiwa kati ya mabunge ya kaunti na ofisi za magavana.

Wanawake wakichota maji kutokana na manufaa ya ugatuzi {picha kwa hisani}
Matokeo ya mizozo hiyo mara nyingi yamekuwa kushuhudiwa kwa mapinduzi katika usimamizi wa ofisi za magavana kupitia hoja za kutokuwa na Imani nazo, au kutokuwa na Imani na usimamizi wa mabunge ya kaunti na Maspika wa mabunge hayo, hatma yake ikiwa ni kushinikizwa kutimuliwa kutoka ofisi zao.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

