Connect with us

News

Panda shuka za kiuongozi katika serikali za ugatuzi

Published

on

Huku Kongamano la Ugatuzi awamu ya 12 likiendelea kaunti ya Homa Bay, bado Wakenya wanaendelea kutathmini iwapo malengo ya ugatuzi yanatimizwa.

Yapo maswali mengi tu kuhusu ufanisi wa kimaendeleo na utenda kazi wa serikali za kaunti ambazo hadi sasa nyingi zao zinazidi kulaumiwa kwa kuendeleza ufisadi, usimamizi mbaya wa rasilimali, na utoaji wa huduma duni, suala ambalo limeendelea kuwamulika magavana na maafisa wengine wa serikali za kaunti.

Tangu Ugatuzi uanzishwe baada ya katiba mpya ya mwaka 2010, Bunge la seneti limetenga takribani shilingi trillioni 4 kwa serikali za ugatuzi kupitia mfumo wa ugavi wa rasilimali za serikali kwa huduma za kaunti, ingawa bado kuna maswali mengi kuliko majibu kuhusu malengo yaliyokusudiwa sheria hii ya ugatuzi.

Uongozi wa serikali hizi bado upo kwenye mizani na mitihani mingi tu, ikiwa ni pamoja na ahadi nyingi zinazotolewa na viongozi wa serikali hizi za kaunti ambazo hazitimizwi kutokana na kile wananchi wanadai ni ukiritimba unaotokana na uongozi mbaya, ufisadi na upendeleo katika utoaji wa huduma na kandarasi.

Suala la utoaji wa kandarasi limekuwa donda sugu katika serikali nyingi za kaunti, huku zikiendelea kukabiliwa na malimbikizi ya madeni.
Miongoni mwa sekta zinazotajwa kuathirika zaidi na usimamizi mbaya au ufujaji wa pesa za umma ni sekta ya afya ambayo. Hospitali nyingi hazina dawa huku huduma za afya zikiendelea kudorora kuanzia ngazi za zahanati hadi hospitali kubwa za kaunti.

Serikali za kaunti pia zinashtumiwa kwa kuendelea na uratibu wa miradi hewa katika bajeti zao, na kupelekea kupotea kwa mabilioni ya pesa za uma.

Japo Ugatuzi ulilenga kuboresha maisha ya Wananchi katika ngazi za chini, bado umaskini umekithiri huku mizozo ya uongozi na utawala wa kibepari vikiendelea kushuhudiwa kati ya mabunge ya kaunti na ofisi za magavana.

Wanawake wakichota maji kutokana na manufaa ya ugatuzi {picha kwa hisani}

Matokeo ya mizozo hiyo mara nyingi yamekuwa kushuhudiwa kwa mapinduzi katika usimamizi wa ofisi za magavana kupitia hoja za kutokuwa na Imani nazo, au kutokuwa na Imani na usimamizi wa mabunge ya kaunti na Maspika wa mabunge hayo, hatma yake ikiwa ni kushinikizwa kutimuliwa kutoka ofisi zao.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending