National News
Zoezi la Kuwapiga Msasa Makishna Wapya Kuanza Mwezi Machi
Jopo la uteuzi wa Makamishna wapya wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, limesema zoezi la kuwahoji na kuwapiga msasa wakenya waliotuma maombi ya kutafuta nafasi hizo litaanza rasmi mwezi Machi.
Mwenyekiti wa Jopo hilo Dkt Nelson Makanda amesema zoezi hilo litafanyika kwa wiki mbili kwani tayari mda wa kutuma maombi ya wale wanaotaka kujaza nafasi hizo ulikamilika Februari 15 mwaka huu na watu 1,848 wametuma maombi yao.
Dkt Makanda amewahakikishia wakenya kwamba zoezi hilo litakuwa huru na haki na litazingatia maadili, sheria na muongozo wa Katiba, huku akisema ni lazima wakenya wapate makamishna wa IEBC walio waadilifu na wachapa kazi.
Dkt Makanda amesisitiza kwamba taifa la Kenya linahitaji makamishna wa IEBC ambao wako tayari kufanikisha uchaguzi huru na haki, bila ya kushurutishwa na wanasiasa ama viongozi walio na ushawishi nchini.
Jopo hilo hata hivyo liko na mda wa hadi tarehe 25 mwezi Aprili mwaka huu, kukamilisha zoezi hilo na kuwasilisha majina ya makamishna wapya wa IEBC kwa rais William Ruto kabla ya kuwasilishwa bungeni ili kuidhinishwa rasmi.
National News
Umoja wa mataifa wapunguza bajeti yake kwa bola milioni 577
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amependekeza kupunguzwa kwa bajeti ya umoja huo ya mwaka ujao kwa dola milioni 577, hatua ambayo itapunguza asilimia 18 ya kazi.
Akizungumza mbele ya kamati ya bajeti ya Baraza kuu la umoja wa mataifa, Guterres alisema umoja huo bado haujapokea mchango wa karibu dola milioni 900 kutoka kwa wanachama mwaka huu wa 2025.
Umoja wa mataifa unapendekeza bajeti ya dola bilioni 3 kwa mwaka 2026, ikiwa na upungufu wa asilimia 15 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka huu.
Umoja wa Mataifa unakabiliwa na mgogoro wa kifedha uliosababishwa pakubwa na hatua ya Marekani kutolipa ada yake, kutokana na sera mpya za Rais Donald Trump.
Hatua hii ya umoja wa mataifa huenda ukachangia changamoto kubwa kwa mataifa wanachama hasa yanayotegemea pakubwa juhudi za umoja huo katika masuala mbalimbali ikiwemo usalama.
Editor's Picks
Bangi Yanaswa Daraja la Sabaki – Malindi, Kaunti ya Kilifi
Maafisa wa Usalama wamenasa shehena ya Bangi katika daraja la Sabaki, Mjini Malindi Kaunti ya Kilifi, iliyokuwa imefichwa kwenye makasha ndani ya basi lililokuwa likisafiri kitoka Lamu kwenda Mombasa.
Basi hilo lilisimamishwa na Maafisa wa usalama katika kizuizi Cha Polisi kilichoko daraja hilo kwa shughuli ya kawaida ya ukaguzi wa magari na mizigo, ambapo magunia mawili ya bangi hiyo yalipatikana yamefichwa katika sehemu ya Mizigo ndani ya basi hilo.
Dereva na Kondakta wa basi hilo, mali ya kampuni ya mabasi ya Tawakal, walikamatwa, ingawa abiria anayeaminika ndiye mwenye kusafirisha bangi hiyo alitotoka mtego huo na bado anatafutwa na Maafisa Polisi.
Waliokamatwa sasa wanazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Mjini Malindi huku uchunguzi zaidi unapoendelea.
Maafisa hao wanasema, walipata vidokezo kuhusiana na bangi hiyo ambayo bado haijajulikana thamani yake.
Katika siku za hivi karibuni, Daraja hilo la Sabaki limekuwa chini ya oparesheni kali ya maafisa wa usalama kutokana kuongezeka Kwa idadi ya vyombo vya usafiri, hasa Malori ambayo yaaminika kutumika kwa zaidi kwa biashara haramu kutoka Kaunti za Tana River na Lamu kuingia Kaunti za Kilifi na Mombasa.
Dereva huyo na Kondakta wake watafikishwa mahakamani hivi karibuni huku maafisa wa Polisi wakitia wito kwa wanachi kutoa habari zitakazosaidia kumtia nguvuni mshukiwa mkuu.

