News
Polisi wamjeruhi mchuuzi kwenye maandamano Nairobi
Maafisa wa polisi wa kupambana na ghasia siku ya Jumanne 17, Juni 2025 walimfyatulia risasi mchuuzi mmoja aliyekuwa akiuza barakoa karibu na barabara ya Moi katikati mwa jiji la Nairobi wakati wa maandamano ya vijana wa Gen Z, yakutaka Naibu Inspekta jenerali wa polisi Eliud Lagat ajiuzulu.
Katika video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii, maafisa wawili wa polisi walionekana wakimkandamiza mchuuzi kando ya barabara ya Moi jiji humo na kuanza kumshushia kipigo.
Mmoja wa maafisa hao alishika bunduki na kumpiga risasi mtu huyo kwa karibu kabla ya kuondoka eneo la tukio.
Kufuatia tukio hilo, wasamaria wema kadhaa walionekana wakiwa wamembeba mtu huyo ili kunusuru maisha yake.
Video hiyo tangu wakati huo imeibua hisia miongoni mwa wakenya huku wakitaka haki itendeke dhidi ya ukatili wa polisi.
Rais wa Chama cha mawakili nchini LSK Faith Odhiambo, pia aliitaja hali hiyo kama isiyokubalika.
Waandamanaji katika miji mbali mbali nchini waliendelea na maandamano ikiwemo jijini Mombasa na mjini Kilifi, wakimshinikiza naibu inspekta mkuu wa polisi Eliud Lagat kujiuzuli kabisa, baada ya kutangaza kujiuzulu kwa mda siku ya jumatatu juni 16 wakati alipohusishwa na mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang’.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

