Connect with us

News

Rais Ruto: Mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu utaendelea

Published

on

Rais William Ruto amesema lengo kuu la serikali ya Kenya kwanza ni kuhakikisha wakenya wananufaika kimaendeleo na wala sio siasa za vurugu na migawanyiko.

Rais Ruto alisema mpango wa kujenga nyumba za bei nafuu katika maeneo mbalimbali nchini utaendelea ili kuhakikisha wakenya wanamudu gharama ya maisha kwani watakuwa na nafasi nzuri kwenye makaazi bora.

Akizungumza jijini Nairobi, Rais Ruto alisema viongozi wengi wamebali kushirikiana na serikali akiwemo Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga ili kuhakikisha wakenya wanafaidi na raslimali zao.

Kiongozi wa nchi, aliweka wazi kwamba atahakikisha miradi yote ya maendeleo nchini inatekelezwa kupitia ushirikiano wa viongozi na wananchi, huku akiwakosoa wale wanajaribu kurudisha nyuma juhudi za maendeleo.

“Tuko na mpango wa kujenga nyumba za bei nafuu kwani wananchi wetu, watu wengi wanaisha katika nyumba duni na alisema hii maneno tutafanya hata wale wengine waongee maneno mengi mimi nitahakikisha natekeleza jukumu langu”, alisema rais Ruto.

Wakati uo huo aliahidi wakenya kwamba serikali itaendelea na mpango wake wa bima ya afya ya jamii SHA, ili kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini wanapata matibabu bila ya kuanganishwa huku akiwarai wakenya kujisajili na SHA.

“Kila mkenya ni lazima apate matibabu kwa gharama ya chini ndio tunasema ni vuzuri wakenya wajisajili katika SHA na tayari wale ambao waliweza kujisajili wameona manufaa ya SHA na kweli tumesajili watu zaidi ya milioni 20”, aliongeza Rais.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending