Connect with us

News

Rais Ruto: Sina mipango ya kuongeza miaka ya uongozi

Published

on

Rais William Ruto amevunja kimya chake kuhusu hatamu ya uongozi na kuwakosoa wale wanaoshinikiza kuendelea kusalia madarakani kwa miaka 20 licha ya Katiba ya Kenya kuweka wazi kwamba hatamu ya rais ni mihula miwili.

Rais Ruto aliwataka viongozi kuondoa fikra hizo na kuangazia maendeleo, akisema wadhfa wa urais sio kitu rahisi vile baadhi ya viongozi wanavyofikiria na kwamba wadhfa huo una changamoto nyingi.

Akizungumza jijini Nairobi, Rais Ruto alisema mda wake wa uongozi ni mihula miwili na utakapokamilika basi ataondoka madarakani na kumuachia kiongozi wengine atakayechaguliwa na wakenya kuwa rais kwa kuzingatia kanuni na sheria za nchi.

“Kuna watu wengine wako na tabia mbaya, wakaenda wakasema huyu mtu amesema atakuwa rais miaka ishirini kwani watu wanafikiria hii kazi ya rais ni kazi rahisi ya kupigiwa kelele kila siku, mimi nangojea siku nitatoka hapa niende mwengine achukue asonge ama namna gani”, alisema rais Ruto.

Kauli yake ilijiri baada ya viongozi mbalimbali nchini hasa wale wanaoegemea upande wa serikali wakiongozwa na Seneta wa Nandi Samson Cherargei, wakipendekeza kubadilisha baadhi ya vipengele vya Katiba ili kuruhusu hatamu ya uongozi kurefushwa hadi miaka 7 badala ya miaka 5 kwa mujibu wa Katiba ya Kenya.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending