News
Rais Ruto: Tumeweka mikakati kuimarisha maendeleo Pwani
Rais William Ruto amesema wanaendeleza mikakati thabiti katika kuhakikisha kuna miradi mingi ya maendeleo ambayo inatekelezwa kaunti ya Kilifi na kanda ya Pwani kwa jumla.
Rais Ruto ambaye aliwahutubia waombolezaji katika hafla ya mazishi ya Gedion Baya Mung’aro ambaye ni babake gavana wa kaunti ya Kilifi, Gedion Maitha Mung’aro eneo Dabaso katika wadi ya Watamu, alisema shilingi bilioni 3 zimetengwa kufanikisha mradi wa umeme kutoka Malindi kupitia Weru hadi Kilifi.
Rais Ruto pia alisema zaidi ya nyumba elfu 20 zitaunganishwa na mradi wa umeme na pia shilingi bilioni mbili na laki mbili zimetolewa kuhakikisha hilo linafanikishwa.
“Ni jukumu la serikali kuu kuhakikisha kila eneo hapa nchini linatekelezewa miradi ya maendeleo bila kutengwa na pwani ni miongoni mwa maeneo hayo ambayo yanafaa kupata maendeleo’’ Alisema Rais Ruto
Wakati huo huo, Rais Ruto akizungumzia bima ya afya ya SHA, alisema hakuna mkenya ambaye atakosa kutibiwa hospitalini kutokana na ukosefu wa fedha na kuwashinikiza wenyeji wa kaunti ya Kilifi na Wakenya kwa jumla kujisajili kwenye bima hiyo ili watibiwe bila changamoto zozote.
“Tunasema matibabu ni haki ya kila mkenya sababu katiba ndio inasema hivyo’’ Alisema Rais Ruto.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

