News
Rais Ruto: Wazazi tuchunge watoto wetu
Rais William Ruto amewashauri wazazi kote nchini kuhakikisha wanawalekuza vijana wao katika mazingira ya maadili na uwajibikaji na wala sio kuwasukuma katika maisha ya kuhangaika.
Rais Ruto aliwahimiza wazazi, viongozi wa kisiasa na kidini kuhakikisha vijana wanazingatia maadili mema, kuwapa mazingira bora na kuhakikisha wanajitenga na makundi potovu.
Akizungumza baada ya kuhudhuria Ibada ya Jumapili katika Kanisa ya AIC Bomani katika kaunti ya Maachakos, Kiongozi wa nchi, alihimiza ushirikiano wa viongozi wote nchini ikiwemo wa kidini ili kuhakikisha wanawalida vijana kwani na nguzo kuu ya taifa.
“Watoto wetu ni zawadi kutoka kwa Mungu kwa familia zetu na taifa. Ni lazima tuwaelekeze, uzazi jukumu ulilopewa na Mungu”, tuachie Kanisa au serikali pekee jamani na tusikubali kuruhusu mtoto wako alelewe na wapiti njia”, alisema Rais Ruto.
Wakati huo huo aliwarai viongozi wa kisiasa kutowachochea vijana na kuzua vurugu sawa na kuharibu mali ya umma, akisema ni jukumu la wazazi, viongozi wa kidini na kisiasa kuwaelekeza vijana katika mwongozo bora.
Kauli yake imejiri baada ya taifa kuhushudia baadhi ya vijana wakipoteza maisha yao baada ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi wakati wa makabiliana kati ya polisi na waandamanaji katika maeneo mbalimbali ya taifa.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

