Connect with us

International News

Rais wa Malawi Chakwera akubali kushindwa katika uchaguzi

Published

on

Rais wa Malawi Lazarus Chakwera amekubali kushindwa katika uchaguzi wa wiki jana, akisema katika hotuba yake kwa taifa kwamba ni wazi mpinzani wake Peter Mutharika alikuwa na “uongozi usioweza kushindwa”.

Mchungaji huyo wa zamani alichukua mamlaka katika uchaguzi wa 2020 alipomshinda rais wa wakati huo Mutharika, ambaye ni mtaalamu wa sheria za kikatiba kutoka chama cha Democratic Progressive Party.

“Dakika chache zilizopita, nilimpigia simu profesa Mutharika kumtakia heri,” Chakwera alisema saa chache kabla ya halmashauri ya kusimamia uchaguzi kutangaza matokeo ya mwisho ya uchaguzi wa Septemba 16, 2025.

Kabla ya tangazo hilo, “ilikuwa wazi kwamba mpinzani wangu Peter Mutharika ana uongozi usioweza kushindwa juu yangu,” alisema Chakwera, mwenye umri wa miaka 70, kutoka Chama cha Malawi Congress (MCP).

Hali mbaya ya uchumi ilitawala uchaguzi katika nchi hiyo ndogo ya kusini mwa Afrika, huku wakosoaji wakimshutumu Chakwera kwa usimamizi mbaya na kutokuwa na maamuzi, na pia kushindwa kukabiliana na ufisadi na kutekeleza ahadi za kuunda nafasi za kazi.

Rais wa Malawi Lazarus Chakwera wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu.

Wakati wa muhula wake, gharama zilipanda katika taifa hilo linalotegemea kilimo, mfumuko wa bei ukifikia asilimia 33 huku bei ya mahindi ya chakula na mbolea ikiongezeka, suala lililokuwa kuu katika uchaguzi huo.

“Katika siku zilizosalia, nataka mjue kuwa nimejitolea kukabidhi madaraka kwa amani, ninajua kwamba wengi wenu mliounga mkono kampeni yangu ya kuchaguliwa tena mtasikitishwa.” Chakwera alisema

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

International News

Rais wa Cameroon amteua mwanawe kuwa makamu wa rais

Published

on

By

Taifa la Cameroon limeidhinisha mabadiliko ya kisheria kuhusu wadhfa wa makamu wa rais na kumpa mamlaka zaidi rais wa taifa hilo kufanya uteuzi upya.

Sheria hiyo mpya, inampa uwezi makamu wa rais kuchukua nafasi ya rais moja kwa moja iwapo rais wa taifa hilo amefariki ama amekubwa na ugonjwa na kushindwa kuendelelea na majukumu yake kama rais kabla ya uchaguzi kuandaliwa.

Bunge la taifa hilo siku ya Jumamosi liliidhinisha mabadiliko hayo ya kisheria na kutoa nafasi ya kuteuliwa kwa makamu wa rais ili kuhakikisha shughuli za kiserikali zinaendeshwa vyema baada ya bunge la kitaifa na seneti kupiga kura na kufanya mabadiliko hayo ya kisheria katika taifa hilo la Cameroon.

Wabunge wa bunge la kitaifa na Seneti nchini Cameroon walipiga kura 200 huku wengine 18 wakipinga na wengine 4 wakikwepa kikao hicho cha bunge, hatua iliyopelekea mswada huo kupitishwa.

Hatua hiyo sasa imefanya Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 kumteua mwanawe Franck Emmanuel Biya kuwa makamu wa kwanza wa rais katika taifa hilo.

Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 na mwanawe Franck Emmanuel aliyemteua kuwa makamu wa rais wa taifa hilo.

Ni hatua ambayo imeibua mjadala mkali nchini Cameroon na bara Afrika kwa jumla baada ya uteuzi huo kutangazwa rasmi Aprili 4, 2026.

Sheria hiyo pia imepiga marufuku wananchi wa taifa hilo kujadili kuhusu hali ya afya ya rais Biya, kukosoa utendakazi wake pamoja na maamuzi yanayofanywa na Ikulu ya rais.

Emmanuel amehudumu katika wadhfa wa mkuu wa majeshi mbali na kushikilia cheo kikuu katika wizara ya ulinzi nchini humo.

Rais Biya amekuwa mamlakani tangu 1982 na alishinda muhula wa nane kwenye uchaguzi mkuu mwaka uliopita.

Kuidhinishwa kwa mabadiliko haya ya kisheria nchini Cameroon kunatambulika kama tukio la kihistoria tangu mwaka 2008 ambapo taifa hilo lilishuhudia pingamizi za kisheria kutoka kwa wananchi baada ya bunge la kitaifa kuongeza hatamu ya uongozi wa rais na kusababisha maandamano makubwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending