Connect with us

News

Serikali yafidia wakaazi wa mzozo wa Wanyamapori milioni 60

Published

on

Serikali ya kitaifa kupitia Wizara ya Utalii na wanyamapori nchini imetoa kima cha shilingi milioni 60 za fidia kwa wakaazi walioathirika na mizozo ya wanyamapori katika kaunti ya Kilifi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kutoa fedha hizo katika wadi ya Marafa eneo bunge la Magarini, Waziri wa Utalii nchini Rebecca Miano alisema fedha hizo zitafidia visa zaidi ya 1,300 vya watu walioathirika na mizozo hiyo tangu mwaka 2021 kaunti ya Kilifi.

Miano alikariri kwamba mizozo ya Wanyamapori kaunti ya Kilifi imeathiri sana maeneo ya Magarini, Ganze na Vitengeni na kuchangia uharibifu wa mimea na hata maafa, akidai kwamba serikali imeweka mikakati kabambe ya kukomesha mizozo hiyo.

Kwa upande wake Naibu gavana wa Kilifi Flora Chibule alielezea matumaini ya kupatikana kwa suluhu la kudumu kwa mizozo hiyo hasa kutokana na mikakati iliyowekwa na serikali ili kutatua suala hilo.

Viongozi na wakaazi katika mkutano wa fidia ya wanyamapori

Wakati huo huo serikali imefichua kuwa imeweka kikosi maalum cha dharura cha maafisa wanaoshughulikia visa vya uvamizi wa wanyamapori kaunti ya Kilifi ikilenga kukabiliana na visa hivyo ili kulinda maisha ya wakaazi.

Haya yanajiri huku tayari serikali ya kitaifa ikiwa imetoa jumla ya shilingi bilioni 2.8 kote nchini za fidia kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori katika awamu ya kwanza huku shilingi bilioni 1.36 zikitarajiwa kutolewa siku zijazo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending