Connect with us

International News

Trump asema Marekani itasitisha vita dhidi ya Iran

Published

on

Rais Donald Trump amesema kwamba Marekani itaondoka Iran hivi karibuni na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo.

Rais Trump alisema Marekani imefikia malengo iliyojiwekea kabla ya kuanza kwa mashambulizi ya anga dhidi ya Iran mwezi uliyopita kwa ushirikiano na Israel.

Aidha aliongeza kuwa lengo la kuizuia Iran kuwa na uwezo wa kuunda silaha za nyuklia limefikiwa na sasa Marekani inamaliza kazi.

Trump pia aliema Marekani sasa inatawala anga za Iran na pia imepata mabadiliko ya utawala kufuatia mauaji ya viongozi wakuu wa kisiasa na kijeshi.

Aliwataja viongozi hao wapya mjini Tehran kama walio na misimamo mikali na waadilifu zaidi, ikilinganishwa na watangulizi wao.

Trump pia alisema viongozi wa Iran wanaomba kufanya makubaliano na Marekani ili kumaliza vita, madai ambayo hapo awali yalipingwa na Iran na kuongeza kwamba vita vinaweza kumalizika bila makubaliano kati ya pande hizo mbili.

Kuhusu athari za vita hasa kupanda kwa bei ya mafuta, rais Trump alisema bei itashuka mara tu Marekani itakapomaliza hatua zake za kijeshi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Vita vya Iran vyasambaratisha biashara za kimataifa.

Published

on

By

Vita vya Iran vinaweza kuisha hivi karibuni au kuendelea kwa miezi kadhaa licha ya tamko la rais wa Marekani Donald Trump kuhusu mpango ya kumaliza vita hivyo.

Iwapo vita hivyo vitakomeshwa basi Hormuz itakapofunguliwa tena ilhali mtihani halisi utakuwa ni vipi minyororo ya usambazaji wa nishati, mbolea na bidhaa nyingine itaweza kurejea haraka.

Wakati wale wenye matumaini wakianza kuhisi kwamba vita kati ya Marekani na Israel dhidi ya Iran vilikuwa karibu kumalizika, mgogoro huo wa mwezi mzima unachukua mwelekeo mwingine tena.

Rais wa Marekani Donald Trump alionya Tehran kwamba hakutakuwa na kurudi nyuma kuhusu mashambulizi yaliyoongozwa ya Marekani, kinyume na kauli yake kwamba hivi karibuni Marekani itaondoka Iran na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo.

Iran, kwa upande wake, inaruhusu idadi ndogo ya meli kupita katika Mlango wa Hormuz, huku ikikanusha kuwa mazungumzo yoyote ya kusitisha vita yanaendelea.

Wataalamu wengi wanakubaliana juu ya jambo moja muhimu: kadiri mzozo huu unavyoendelea kwa muda mrefu, ndivyo athari zake zitakavyokuwa mbaya zaidi kwa usambazaji wa nishati duniani, mfumuko wa bei na uthabiti wa uchumi.

Benki ya hifadhi ya Shirikisho ya Dallas, ambayo ni sehemu ya mfumo wa benki kuu ya Marekani, ilitabiri mapema mwezi huu kwamba kufungwa kwa mlango huo kwa miezi mitatu au zaidi kungesababisha ukuaji wa pato la taifa la dunia kupungua kwa asilimia 2.9 kwa mwaka katika robo ya pili ya mwaka.

Continue Reading

International News

Bunge la Israel limepitisha sheria mpya ya adhabu ya kifo

Published

on

By

Bunge la Israel limepitisha sheria mpya inayotoa adhabu ya kifo kwa Wapalestina watakaopatikana na hatia ya mashambulizi ya mauaji dhidi ya Waisrael.

Sheria hiyo ilipitishwa kwa kura 62 dhidi ya 48, huku mbunge mmoja akijizuia kupiga kura na wengine kutohudhuria kikao hicho.

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alihudhuria kikao hicho na kupiga kura kuunga mkono mswada huo bungeni.

Mswada huo wa sheria uliwasilishwa na Waziri wa usalama wa taifa hilo Itamar Ben Gvir, ambaye ni mmoja wa wanasiasa wenye msimamo mkali nchini humo.

Hatua hiyo imeibua mjadala mkubwa wa kimataifa, huku mataifa ya Umoja wa Ulaya na mashirika ya haki za binadamu yakielezea wasiwasi mkubwa.

Muda mfupi baada ya kupitishwa, kundi la haki za binadamu la Israel lilisema limewasilisha malalamiko katika Mahakama kuu ya nchi hiyo.

Mamlaka ya Palestina ilitaja mswada huo kama uhalifu wa kivita dhidi ya watu wa Palestina, ikisema kwamba unakiuka mkataba wa Geneva.

Hata hivyo mamlaka ya Washington ilisema kwamba Israel ina haki ya kutungu sheria zake huku nchi zikiwemo Ujerumani, Ufaransa, Italia na Uingereza zikielezea wasiwasi mkubwa kuhusu mswada huo.

Continue Reading

Trending