Connect with us

International News

Upinzani Sudan Kusini watoa wito wa vikosi kukusanywa kwa ajili ya ‘mabadiliko ya serikali’

Published

on

Upinzani nchini Sudan Kusini ulitoa wito Jumatatu 15, Septemba 2025, wa uhamasishaji wa silaha kufanya “mabadiliko ya serikali” ili kukabiliana na mipango ya kumweka kiongozi wake mahakamani kwa makosa ya uhaini na uhalifu dhidi ya ubinadamu.

Mkataba dhaifu wa kugawana madaraka kati ya rais Salva Kiir na mpinzani wake wa muda mrefu, Riek Machar, umekuwa ukisuasua kwa miezi kadhaa, na kutishia kurejesha taifa hilo changa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyosababisha vifo vya watu 400,000 katika miaka ya 2010.

Siku ya Alhamisi, Machar alishtakiwa kwa kosa la mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya ubinadamu na kuvuliwa wadhifa wake kama makamu wa kwanza wa rais katika serikali ya muungano, akiwa tayari amekaa miezi kadhaa chini ya kifungo cha nyumbani.

Alishtakiwa kwa kuamuru shambulio la wanamgambo wa kikabila kwenye kambi ya kijeshi mnamo Machi 2025, ambayo serikali ilisema iliua zaidi ya wanajeshi 250.

Mrengo wa Machar ulikanusha mashtaka hayo na ulisema ni sehemu ya juhudi za Kiir kuweka kando upinzani na kuimarisha mamlaka.

“Utawala wa sasa… ni muundo wa udikteta, wavunjifu wa amani na utekaji nyara wa serikali ambao unashikilia mamlaka kinyume cha sheria na kwa vurugu,” chama chake kilisema katika taarifa iliyotiwa saini na kaimu mwenyekiti Oyet Nathaniel Pierino na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Chama na vikosi vyake “vitafanya kazi katika Jamhuri ya Sudan Kusini mabadiliko ya serikali”, ilisema taarifa hiyo, ikitoa wito kwa wafuasi wote “kuripoti kwa Jeshi la Kitaifa ili kulinda raia na nchi”.

Sudan Kusini ilipata uhuru wake kutoka kwa Sudan mwaka 2011 lakini ikatumbukia katika mzozo mkubwa kati ya Kiir na Machar.

Vita vya miaka mitano vilimalizika kwa makubaliano ya amani mwaka 2018 lakini majaribio ya jumuiya ya kimataifa kuhakikisha mabadiliko ya kidemokrasia yameshindwa.

Uchaguzi uliopaswa kufanyika Desemba 2024 uliahirishwa tena hadi 2026 na pande hizo mbili hazijaunganisha vikosi vyao vya kijeshi.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Vita dhidi ya Al-Shabab vya shika kasi Somalia

Published

on

By

Operesheni kali ya kijeshi inayoendelea nchini Somalia ambapo zaidi ya wanamgambo 33 wa kundi la Alshabab wameuawa katika eneo la Shabelle nyanda za chini za Jubaland.

Ufanisi wa operasheni hii ya hivi punde ni muendelezo wa oparesheni iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Aprili 24 katika eneo hilo la Juba ambapo Wanamgambo 27 wa AlShabab waliuawa.

Hii ina maana kwamba Jeshi la Somali limefanikiwa kuvunja maficho muhimu ya kundi hilo, ambalo kufikia sasa ya Wanamgambo 60 wameuawa

Kwa mujibu wa vianzo vya habari hususan kutoka kwa maafisa wa usalama, operesheni hiyo inafanyika kufuatia taarifa za kijasusi kuhusu maficho ya wanamgambo hao waliokuwa wakipanga mashambulizi dhidi ya vituo muhimu na taasisi za serikali.

Wanajeshi hao walivamia ngome za magaidi hao kwa ustadi mkubwa, wakifanikiwa kudhibiti eneo hilo baada ya mapambano makali yaliyochukua muda wa saa kadhaa.

Maafisa wamesema kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuimarisha usalama na kuangamiza kabisa mtandao wa Al-Shabaab ambao kwa muda mrefu umekuwa ukihatarisha amani katika maeneo mbalimbali ya Somalia na ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Wananchi wa eneo la Jubbaland wameelezea matumaini mapya kufuatia operesheni hiyo, wakisema kuwa hatua hiyo inaleta nuru ya kurejea kwa utulivu na maendeleo baada ya miaka ya hofu na mashambulizi ya mara kwa mara nchini.

Serikali imeapa kuendeleza msako dhidi ya wanamgambo hao hadi pale watakapokomesha kabisa vitisho vya mashambulio , huku ikiwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kudhibiti ugaidi.

Taarifa ya Billy Mongo

Continue Reading

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending