Connect with us

News

Viongozi wa dini wamkosoa Kithure Kindiki.

Published

on

Viongozi wa dini ukanda wa wamemkosoa naibu rais profesa Kithure Kindiki kuhusiana na kauli yake kwamba baadhi ya viongozi wa dini na wanadiplomasia walihusika katika kuunga mkono maandamano ya vijana wa kizazi cha Gen Z ya mwezi juni 25 2025.

Mwenyekiti wa kitaifa wa baraza la kuu la waislamu SUPKEM Sheik Muhdhar Khitamy alisema matamshi ya Kindiki ni siasa zinazolenga kuwanyooshea lawama viongozi wengine.

Sheikh Kitamy alisema kuwa kwa sasa wanasiasa wamekuwa na usemi mkubwa kutokana na hulka ya kuwahonga wananchi na kuwafanya viongozi wa dini kutosikizwa.

Akizungumza na wanahabari kiongozi huyo wa dini ya kiislamu alionya kuwa  iwapo wakenya hawatakuwa makini, kunauwezekano wa taifa kuelekea pabaya kutokana na vijana kutumiwa vibaya na wanasiasa.

“Ukweli wa mambo ni kwamba wanasiasa wanachukuwa jukumu kubwa sana kwa sababu ya pesa za kuwatumia watu, jambo lolote liwe la kikatiba au nini utaona linawahusisha hao wanasiasa, twawaambia wanasiasa hao ndio chumvi, watengeneze nchi, watakuja kujuta kwasababu hali inavyokwenda ni mbaya”, alisema Khitamy.

Naye mwakilishi wa vijana katika baraza hilo Abdhulmalik Ali aliwataka vijana nchini kuwa makini na kufuata ushauri wa kisheria iwapo hawajaridhishwa na utendakazi wa viongozi.

Ali vile vile aliwashinikiza vijana kuepuka maandamano ya vurugu.

“Wanasiasa tuchungane nao, niwatu wanamaslahi yao zaidi ya wewe kijana, hii kenya inakuhitaji wewe kijana, kama kiongozi anatufaa tumpigie kura muhula ujao, kama hatufai njia iko ya kumtoa lakini sio suala la kumwaga damu”, alisema Abdhulmalik.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending