Connect with us

News

Viongozi wa jamii ya Mijikenda wakosoa maandazili ya sherehe za Chenda chenda.

Published

on

Baadhi ya viongozi wa jamii ya mijikenda eneo la pwani wamekosoa mpangilio wa sherehe za kitamaduni za jamii ya kimijikenda maarufu chenda chenda zilizofanyika jana Kaunti za Kilifi na Kwale.

Wakiongozwa na mwenyekiti ya baraza la jamii ya Chonyi Raphael Mwangala walisema msingi wa maandalizi ya sherehe hizo ni mshikamano ya jamii ya Mijikenda na wala sio mgawanyiko kama ilivyoshuhudiwa hapo jana.

Mwangala alisema taswira iliyojitokeza hapo jana hairidhishi kwa wamijikenda na inaonyesha hawana msimamo.

“Walioanzisha hii chenda chenda si lengo la kugawanyana, ni lengo la kuja pamoja, wengine wanachukua tu ni chenda chenda mijikenda waje wakae tu, lakini leo yule anaenda fanya Kwale, yule anaenda fanya wapi, hilo sio lengo, ningewasihi Mijikenda wenzangu, ngewasihi hata viongozi ambao wanajiita ni viongozi wa chenda chenda wafikirie lazima twende pamoja zi mambo ya kugawanyana”, alisema Mwangala.

Anadai sherehe hizo zimeingiliwa kisiasa akisistiza umuhimu wa kubuniwa kamati mpya ya jamii hiyo itakayohusisha mwakilishi wa kila kabila.

“Kwanza kamati ni wakina nani? Ni lazima kamati iuende mpya ya chenda chenda kwa kila mmijikenda awe mule ndani ya kamati ili wakipanga wawe wanaenda pamoja”, aliuliza Mwangala.

Baadhi ya watumbuizaji wa ngoma za kiasili katika sherehe za chenda chenda mjini Kilifi.

Kwa upande wake gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro Mung’aro aliahidi kuunda kamati maalum itakayohusisha wazee wa Kaya ili kuangazia ulinzi wa misitu ya Kaya.

Akizungumza wakati wa sherehe hizo katika chuo kikuu cha Pwani, Gavana Mung’aro alisema kamati hiyo itahakikisha misitu ya kaya inazunghushiwa uwa ili kudhibiti uvamizi wa binadam.

Kauli ya gavana huyo ilijiri baada ya wazee wa Kaya kulalama kuwa misitu ya Kaya imekuwa ikisambaratika kutokana na uvamizi na kutatiza shughuli za mwendelezo wa mila na tamaduni za wamijikenda.

“Nitaunda kamati ya wazee wa Kaya tuangazia maneno ya misitu na mashamba ili kuwekewa ua ili itunzwe dhidi ya wavamizi,tunatengeneza kitengo cha vijana watyakaokuwa walinzi wa msitu kwa sababu tuiko na wizara hiyo ndani ya kaunti”, alisema Mung’aro

Kwa upande wake katibu katika wizara ya vijana na uchumi bunifu Fikirini Jacobs amesistiza jamii ya mijikenda hasa vijana kuzingatia umuhimu majukumu ya  uongozi waliyonayo katika jamii.

Sherehe hizo ambazo ni makala ya nane kufanyika, ilifaa kufanyika kaunti ya Kwale kulingana na mpangilio wa awali wa kufanyika kile eneo la pwani japo kulifanyika mabadiliko siku za mwisho.

Mwenyekiti wa bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa na gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani kwenye sherehe za Chenda chenda Kwale

Hatua hiyo ilikashifiwa na baadhi ya viongozi ambapo maandalizi mengine yalifanyika katika msitu wa Kaya Mtswakara kaunti ya Kwale ambapo mwenyekiti ya bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa alihudhuria.

Taarifa ya Joseph Jira

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending