News
Visa vya mauji ya wazee vyapungua Kilifi
Idara ya usalama kaunti ya Kilifi imeripoti kupungua kwa visa vya mauaji ya wazee, hatua inayotajwa kuwa mafanikio makubwa katika juhudi za kukomesha uhalifu huo unaochochewa na imani potovu za uchawi.
Kwa mujibu wa kamishna wa kaunti hiyo, Josephat Biwot, idadi ya wazee waliouawa mwaka jana ilishuka hadi watu 12, ikilinganishwa na mwaka wa 2023 ambapo visa 60 vya mauaji viliripotiwa.
Biwot, alisema mauaji hayo hayahusiani moja kwa moja na uchawi kama inavyodhaniwa, bali yanatokana na migogoro ya ardhi, huku ndugu na jamaa wa karibu wa waathiriwa wakitajwa kuwa wahusika wakuu.
“Nikija Kilifi 2023 tulikuwa tunapoteza wazee karibu 60 kwa mwaka, lakini mwaka jana kwa bahati mbayu tu tulipoteza wazee 12 pekee, na wale walikufa kulishika washukiwa wote”,alisema Biwot.
Kamishna huyo aliwaonya vijana wanaojihusisha na vitendo hivyo, akisema serikali haitasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yao.
“Tunaomba vijana wetu hii ni laana, sasa wewe unaua babayako kwa sababu ya shamba, wewe utaishi namna gani? Kwa sababu waweza kuua baba uuze shamba, ununue pikipiki ndio unaona ajali nyingi”, aliongeza Biwot.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

