Connect with us

News

Wahudumu wa Sekta ya Uchukuzi Wanahimiza Ukarabati wa Barabara ya Kibaoni-Ganze-Bamba

Published

on

Wahudumu wa sekta ya uchukuzi mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wanashinikiza serikali kuu na ile ya kaunti kuzingatia ukarabati wa barabara ya Kibaoni-Ganze hadi Bamba licha ya kushinikizwa kusitisha maandamano ya kufunga barabara hiyo.

Wakizungumza na Coco FM, wahudumu hao wamesema barabara hiyo ingali na hitilafu nyingi na wanahofia huenda ikaharibika vibaya msumu huu wa mvua.

Wakiongozwa na Praise Majimbo ambaye ni mhudumu wa bodaboda, wamesema hatua ya kulima barabara hiyo kwa tinga tinga haitoshi kwani bado kuna vumbi na mashimo hali inayowatatiza shughuli zao za kibiashara. 

Kwa sasa kidogo iko na afadhali lakini bado hatujaridhika na kile chenye tunapitia, kwa sababu kwengine kushatengenezwa na mvua imenyesha tayari sasa hivi mashimo yako mengi, vyenye niko tayari nyewe nimechoka kutoka Kakanjuni mpaka barabara vyenye iko kwa ukweli, vumbi na mashimo pia yashaongezeka kwa sababu ya mvua”, alisema Majimbo. 

Nao wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma wakilongozwa na Samson Kitsao Wako, wanasema wanapitia changamoto za kukarabati magari yao kila mara kutokana na hali mbaya ya barabara hiyo.

“Lakini kwa saa tutasema inaafadhali kwa sababu, tuliandamana na tukafunga na baadaye serikali ikaleta tinga tinga ikapiga msasa kutoka hapa Kibaoni mpaka Silala, lakini sasa kutoka Ganze mpaka Bamba ndio barabara ni mbaya sana, mvua ikianza kunyesha tutapata shida sana kwa sababu barabara wakati wa mvua hua inateleza”, alisema Kitsao. 

Vile vile wachuuzi wa vyakula kando ya barabara hiyo Wakiongozwa na Fiki Kenga wanasema idadi ya wateja imekuwa ikipungua kutokana na vumbi linalotoka barabarani kila mara, wakisinikiza serikali kuzingatia kilio chao.

“Tunapata taharuki hata vyakula vyetu huwa haviendi vizuri kila siku, hii barabara ilifanya kukwaruzwa kwaruzwa huko, angalau tusiumizwe na hili vumbi, barabara iko na vumbi wateja wanalalamika kwa sababu vumbi si nzuri kwa chakula, kwa hivyo tunaomba msaada tuwe nasi tutakaa vizuri mahali tuko”, waliongeza baadhi ya wachuuzi.

Aidha wameshinikiza serikali kuangazia matatizo wanayopitia baadhi yao wakidai wanawake wajawazito wamekuwa wakipoteza watoto wachanga hasa wanaposafirishwa kwa pikipiki kuelekea hospitali kujifungua kutokana na ubovu wa barabara hiyo. 

Itakumbukwa kwamba wakaazi pamoja na wahudumu wa uchukuzi wa umma waliandamana na kufunga barabara hiyo kwa majuma kadhaa na kutatiza shughuli za usafiri.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending