Business
Wakaazi wahofia mkurupuko wa magonjwa baada ya kuuziwa nyama Malindi
Wakaazi wa mji wa Malindi kaunti ya Kilifi wanaishi kwa hofu ya mkurupuko wa magonjwa baada ya kulalamikia kuuziwa nyama ya mifugo ambayo haijakaguliwa na maafisa wa mifugo eneo hilo.
Wakielezea manung’uniko yao, wakaazi hao walioongozwa na Kensa Ondiek walisema nyama ya mifugo inayouzwa eneo hilo haijakaguliwa, akiongeza kwamba kichinjio cha kipekee mjini humo pia kina wafanyikazi ambao ni wa umri wa chini ya miaka kumi na nane.
Wakaazi hao pia walisema mazingira ya kufanya kazi katika kichinjio hicho nai ya kutatanisha huku wachuuzi wa nyama wakifanya biashara zao mahali peupe na pachafu.
Vyombo vya Habari vilidhibitisha matukio hayo kupitia picha za watoto wakifanya kazi katika kichinjio hicho na kuchinjwa kwa mifugo siku ya Jumapili.
Afisa wa mifugo eneo la Malindi Godreck Mwaringa alitetea madai hayo akisema kwamba mifugo inayochinjwa katika kichinjio hicho hukaguliwa pindi inapofika, kabla na baada ya kuchinjwa.
Aliongezea kwamba maafisa husika hufanya kazi kuanzia siku ya Jumatatu hadi Jumamosi, japo akaweka wazi kwamba huenda wanaochinjwa siku ya Jumapili huwa ni uchinjaji wa dharura ambao pia nyama yake inafaa kukaguliwa kabla ya kuuzwa.
Hata hivyo alitoa tahadhari kwa wakazi wa Malindi kuhakikisha wananunua nyama iliyokaguliwa huku akionya kuwa watakaopatikana na mifugo wala nyama ambayo hazijakaguliwa watashtakiwa.
Taarifa ya Eric Ponda
Business
Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao
Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.
Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.
Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.
Wanasema wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani zimesalia sokoni kwa muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.
Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.
“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho
Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.
Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.
Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.
Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.
Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.
“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

