Connect with us

News

Maadhimisho ya ugonjwa wa Selimundu duniani

Published

on

Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya ugonjwa wa Selimundu maarufu Sickle cell Aenemia, ukosefu wa hamasa za kutosha miongoni mwa jamii umetajwa kuchangia ongezeko la kusambaa kwa ugonjwa huo hasa maeneo ya Pwani.

Kulingana na Daktari wa watoto wenye ugonjwa wa Selimundu na pia ni mtafiti katika taasisi ya utafiti wa matibabu nchini KEMRI kaunti ya Kilifi Mejumaa Mohammed, amesema kwamba watoto wengi wanaadhirika na ugonjwa huo pasi nao kutambua kwamba wanaugua Selimundu.

Daktari Mejumaa alibainisha kwamba baadhi ya dalili za ugonjwa huo kwa watoto huonekana miezi minne hadi sita baada ya mtoto kuzaliwa.

“Ni jukumu la wazazi kuwa makini na afya ya watoto wao kwani magonjwa mbalimbali ya kuchipuka na kuathiri afya ya mtoto hasa Selimundu huonekana baada ya miezi mine hadi sita na kwamba ni hatari kwa afya ya mtoto kama hutabainika kwa haraka”, alisema Mejumaa.

Msimamizi wa wagonjwa wa magonjwa yasioambukizwa John Mosi, alisema Kilifi ni baadhi ya maeneo yaliothirika pakubwa na ugonjwa huo huku akisema kwamba wazazi walio na chembechembe za ugonjwa wa Selimundu wanapooana huenda wakapata mtoto aliyeadhirika na ugonjwa huo.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending