Connect with us

News

Wakfu wa George Kithi wapata Tuzo za Africa Champions Awards

Published

on

Wakfu wa George Kithi kwa mara nyengine umepata Tuzo za Africa Champions Awards kwa kutambulika kama Shirika linalotegemewa na wengi katika jamii.

Tuzo hizo za Africa Champions Awards ambazo ni Tuzo za kimataifa zilifanyika katika hoteli moja kaunti Mombasa zikilenga kuwapa motisha wadau mbalimbali, mashirika, Wanahabri pamoja na wawekezaji.

Masuala yaliyoangaziwa zaidi na wasimamizi wa Tuzo hizo na ambayo yalichangia Wakfu wa George Kithi kupata Tuzo hizo ni pamoja na juhuzi zinazoendeleza na Wakfu huo za kuiwezesha jamii ya kaunti ya Kilifi kujiimarisha zaidi katika masuala mbalimbali.

Mpango wa hivi majuzi wa kuwasaidia zaidi ya wakaazi 5,000 kutoka kaunti za Pwani kwa matibabu ya bure kwenye kambi ya matibabu ya bila malipo iliyoandaliwa katika uwanja wa chuo kikuu cha Pwani pamoja na ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wasiojiweza, ni kati ya vigezo vilivyoangaliwa na wasimamizi wa Tuzo hizo za Africa Champions Awards.

Wakfu huo pia ulitambulika kwa juhudi zake za kuendelea kuisaidia jamii kujiimarisha kiuchumi kama dhamira ya Mkurugenzi wa Wakfu huo Wakili George Kithi, huku suala la kukuza vipaji na kufungua milango ya mustakabali ulio bora zaidi kwa jamii ukichangia zaidi Wakfu huo kupata Tuzo hizo.

Hata hivyo Wakili George Kithi, alipongeza Waandalizi wa Tuzo hizo za Africa Champions Awards kwa kutambua juhudi zinazoendelezwa na Wakfu wa George Kithi pamoja na mipango na mikakati ya Wakili huyo kwa jamii ya kaunti ya Kilifi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending