News
Wakristu Waadhimisha Siku ya Ijumaa Kuu
Waumini wa Kanisa Katoliki kote ulimwenguni wamejitokeza kuadhimisha ibada ya njia ya msalaba, wakiashiria ukumbusho wa mateso ambayo Yesu Kristu alipitia kabla ya kufa na kufufuka kulingana na imani ya dini hiyo.
Ibada ya njia ya Msalaba, huadhimishwa kila mwaka baada ya waumuni wa Kanisa Katoliki kukamilisha kipindi cha kufunga na kusali ambayo hutambulika kama Kwaresma, kisha Jumapili ya Matawi na hatimaye kipindi cha Pasaka ambayo huanza rasmi na siku ya Ijumaa Kuu.
Kulingana na Kanisa Katoliki, siku ya Ijumaa kuu, ni kipindi cha mwisho cha maisha ya Yesu Kristu kabla ya kuteswa, kufa na hatimaye kufufuka siku ya tatu ambapo waumuni hao kuadhimisha sherehe za sikukuu ya Pasaka.
Viongozi mbalimbali wa kidini katika Kanisa Katoliki la St Patrick Parokia ya Kilifi wakiongozwa na Padre Marsellous Okello, wamehimiza umuhimu wa unyenyekevu na amani jinsi Yesu Kristu alivyoyaweka maisha yake kwa Mungu.
Hata hivyo maafisa wa usalama wameahidi kuimarishwa kwa usalama katika maeneo mbalimbali ya Pwani ikiwemo maeneo ya burudani, fuo za bahari hindi pamoja na vituo vya kuabiri magari ya uchukuzi wa umma.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

