Connect with us

News

Wanaosajiliwa Kwenye Mpango wa Kazi “Majuu” Waonywa.

Published

on

Waziri wa Leba nchini Dakta Alfred Mutua amewaonya vijana waliopata nafasi za ajira ughaibuni dhidi ya kujihusisha na visa vya utovu wa nidhamu.

Akizungumza wakati wa zoezi la kusajili vijana kwenye mpango wa ajira za nje nchi maarufu Kazi “Majuu” katika kaunti ya Kwale, Waziri Mutua alitaja hatua hiyo kwamba huenda ikachangia kandarasi zao kufutiliwa mbali sawa na kukabiliwa kisheria.

Mutua alidokeza kwamba kuna baadhi ya vijana ambao tayari wamerejeshwa nchini kufuatia visa vya utovu wa nidhamu

“Unaskia unawashwa unataka kuandamana, unataka kuwa mwanaharakati, unataka kuchochea ingia ndege uje hapa wikendi moja uandamane kila mahali hiyo kitu ikutoke urejee kazini, kwa sababu ukienda kufanya huko maandamano unaharibia wakenya wengine, kuna watu waliandamana huko nchi tofauti tofauti, wakenya kumi na tano wengi wakasimamishwa, wakaregeshwa nyumbani, unaandamana kwa nchi nyengine wanauliza mbona mkenya anaandamana na mganda haandamani, mbona mtanzania haandamani”, alisema waziri Mutua.

Akizungumzia suala la utumizi wa dawa za kulevya, Waziri Mutua amewataka vijana hao kukomesha uraibu huo kwani  hakuna taifa linaloshabikia matumizi ya dawa za kulevya.

“Hapa utafanyia ukaguzi wa kiafya kama umekuwa ukivuta bangi, madawa ya kulevya utaanguka, hata ukikataa kupatikana hapa ukifika ng’ambo  utapatikana, kwa hivyo kama unataka kwenda ng’ambo achana na bangi bwana”,aliongeza waziri Mutua.

Zoezi hilo lililenga vijana 800 kaunti ya Kwale na 3,500 eneo la pwani kwa ujumla.

Taarifa ya Joseph Jira

 

 

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi yawatupa gerezani washtakiwa zaidi ya 10

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa washtakiwa zaidi ya 10 waliowasilishwa Mahakamani wakikabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwemo kesi za unajisi na makosa ya jinai.

Katika vikao vya Mahakama siku ya Jumatano tarehe 3 June 2026, Hakimu Ivy Wasike ametoa hukumu hizo kwa watuhumiwa hao huku wengine wakifungwa kwa zaidi ya miaka 30 gerezani.

Simon Ngala, Aliwali Ali Mwalimu, Christopher Buru, miongoni mwa wengine zaidi ya 10 walifikishwa katika Mahakama ya Kilifi na kuhukumiwa kufuatia mashtaka mbalimbali yanayowakabili ikiwemo mashtaka ya unajisi na makosa ya jinai.

Hakimu wa Mahakama ya Kilifi Ivy Wasike, alimhukumu kifungo cha miaka 30 gerezani Simon Ngala baada ya kupatikana na hatia ya kumnajisi mtoto wa miaka 13 kisha akamtorosha kwao kwa kipindi cha mwezi mzima.

Mwengine ni Aliwali Ali Mwalimu, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 25 kufuatia mashtaka ya kumpachika ujauzito mtoto wa miaka 13 licha ya kuomba msamaha Mahakamani.

Wakati wa kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisikitishwa na kukithiri kwa visa vya watoto kupotea na kisha kunajisiwa katika kaunti ya Kilifi.

Kiongozi wa mashtaka katika Mahakama hiyo Nancy Njeru alipinga vikali ombi lililowasilishwa Mahakama la kutaka washtakiwa wasamehewe, kwanin wengine walidai kwamba walishirika makosa hayo bila kukusudia, akisema hukumu hizo zitakuwa funzo kwa watu wenye hulka hizo katika jamii.

Mbali na hukumu za kesi za unajisi, Christopher Buru alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani akikabiliwa na mashtaka ya wizi baada ya kupatikana na hatia ya kutumia pesa za mlalamishi Saumu Nyevu aliyekuwa akimtumia pesa alipokuwa akifanya kazi katika milki za kiarabu, kosa lililomchukiza zaidi Hakimu Wasike.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Washukiwa 5 wa uhalifu wanazuiliwa na polisi Likoni

Published

on

By

Maafisa wa polisi katika eneo bunge la Likoni kaunti ya Mombasa wanawazuiliwa washukiwa 5 wa uhalifu waliokamatwa katika oparesheni iliyofanyika maeneo ya Duduz na Bufallo siku ya Jumatatu tarehe mosi Juni 2026.

Washukiwa waliokamatwa ni Brian Musa mwenye umri wa miaka 24, Abubakar Mahasi wa umri wa miaka 20, Juma Kassim mwenye umri wa miaka 16, Omar Gobeko maarufu Mboga mwenye umri wa miaka 19 na Jackson Mwambu mwenye umri wa miaka 26.

Msako huo uliongozwa na mkuu wa kituo cha polisi cha Shelly Beach pamoja na kikosi cha maafisa wa polisi.

Maafisa wa Polisi wamesema mshukiwa Brian Musa anakabiliwa na tuhuma za maandalizi ya kutenda kosa la jinai, huku Ababakar Mahasi, Juma Kassim na Omar Gobeko wakihusishwa na tuhuma za wizi wa mabavu.

Mshukiwa mwengine Jackson Mwambu anahusishwa na tuhuma za kupatikana na mali ya serikali kinyume cha sheria.

Katika oparesheni hiyo, maafisa wa polisi walifanikiwa kupata vielelezo mbali mbali ikiwemo panga tatu pamoja na koti la jeshi la KDF.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending