Connect with us

News

Wapwani watahadharishwa kuhusu mafuriko

Published

on

Idara ya utabiri wa hali ya hewa kanda ya Pwani imetoa tahadhari ya kushuhudiwa kwa mvua kubwa, kuanzia wiki ijayo ya milimita 20 kwa saa 24.

Idara hiyo imezitaja kaunti za Pwani ikiwemo Kwale, Mombasa, Kilifi, Tanariver na Lamu kwamba zitashuhudia mvua hizo pamoja na kusababisha mafurikio, ikiwataka wananchi kuwa waangalifu.

Maeneo yalitojwa kushuhudia mafuriko ni pamoja na eneo la Sultan Hamud, kwenye barabara kuu ya Mombasa-Nairobi, eneo la daraja ya Mbogolo kwenye barabara kuu ya Mombasa-Malindi pamoja na maeneo ya Likoni na Nyali kaunti ya Mombasa.

Wakaazi wanaoishi katika maeneo ya nyanda za chini katika kaunti ya Tanariver na Kwale wahimizwa kuhamia maeneo salama ili kuepuka majanga sawa na kuzingatia mazingira salama na safi.

Wakati huo huo idara hiyo imewashauri wananchi wanaoishi karibu na Mto Tana katika kaunti ya Tanariver kuchukua tahadhari ya mapema na kuhamia maeneo salama kwani huenda mto huo ukavinja kingo zake. 

Hata hivyo Afisa wa Mawasiliano wa Kampuni ya usambazaji maji ya GAWASCO katika kaunti hiyo, Omar Abdullahi alisema huenda wakaazi wa kaunti hiyo wakabiliwa na uhaba wa maji kufuatia mafuriko.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending