Connect with us

News

Waumini wa dini ya kikristo waadhimisha ibada ya majivu

Published

on

Waumini wa Kanisa Katoliki pamoja na waumini wengine wa dini ya kikristo wameungana kote ulimwenguni kuadhimisha ibada ya Misa ya Jumatano ya majivu ishara ya kuanza kwa kipindi cha mfungo wa siku 40 yani Kwaresma.

Padri wa Kanisa Katoliki la St. Patrick mjini Kilifi Henry Ndune alisema kwamba kipindi cha Kwaresma kina ashiria kujinyima kula na kunywa, kujitenga na maovu na dhani pamoja na ushawishi amba0 huenda ukamfanya mwanadamu kutokuwa karibu na mwenyezi Mungu.

Kulingana na Padre Ndune, kipindi cha Kwaresma hukamilika na maadhimisho ya siku ya Alhamis kuu ambapo kuhani huwaosha miguu wanaume 12 kama kumbukumba ambazo Yesu Kristo alifanya kabla ya kuhukumiwa na kufariki.

Siku ya Ijumaa kuu kabla ya ufufuko wa Yesu Kristo ambayo kuadhimishwa kabla ya sikukuu ya Pasaka, huashirikia ukumbusha wa mateso aliyopitia Yesu Kristo kabla ya kifo chake na baada ya siku tatu akafufuka kutoka kwa wafu kulingana na imani ya dini ya kikristo.

Padre Ndune, katika maelezo yake kuhusu kipindi cha Kwaresma alisema sio Kanisa Katoliki pekee linaloadhimisha mfungo wa siku 40,  lakini pia makanisa mengine kufanya hivyo yenye imani ya dini ya kikristo ikiwemo Kanisa Kianglikana.

Padre Ndune alieleza kuwa sababu ya wakristo kuadhimisha ibada ya majivu ni kuashiria unyenyekevu sawa na kukumbushwa kuhusu umuhimu wa kujitenga na ubinafsi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending