Connect with us

News

Wavuvi wataka KPA kumwaga tope eneo mbadala baharini

Published

on

Wavuvi eneo bunge la Likoni, kaunti ya Mombasa, wameitaka halmashauri ya bandari nchini (KPA) kusitisha mara moja shughuli za kumwaga tope maeneo ya bahari wanakofanyia shughuli zao za uvuvi.

Wavuvi hao walisema tope hizo zimeathiri mazingira ya bahari na kuhatarisha maisha ya viumbe hai majini, hasa samaki ambao ni tegemeo lao kuu la kipato.

Wakizungumza wakati wa kikao cha hadhara cha kukusanya maoni ya wananchi kuhusu uandaaji wa mpango wa maendeleo ya kaunti wa mwaka wa fedha 2026/2027 wavuvi hao walieleza kuwa tope hizo zinatokana na upanuzi wa kina cha bandari, na kumwaga tope baharini kunasababisha uchafuzi wa maji na kuharibu mazalia ya samaki.

Wakiongozwa na Shaban Mohammed, waliitaka KPA kushirikiana na jamii za wavuvi kabla ya kutekeleza miradi yoyote inayohusisha maeneo ya bahari, na kutumia mbinu mbadala za utupaji wa tope zinazolinda mazingira na maisha ya wakazi.

“Wale watu wanaokuja kuchimba kula bandarini wanamwaga tope kwenye mazingira ya samakai ambako ndio maeneo tunavua samaki, hatujui ni eneo walipewa na wanaochimba kule au ni wao wenyewe wanafanya hivyo kwa sababu hawafiki mahali stahiki ya kumwaga zile taka”,alisema Mohammed

Aidha, gavana wa Mombasa, Abdulswamad Sharif Nassir, aliahidi kufuatilia suala hilo na taasisi husika ili kuhakikisha linaangaziwa na kutatuliwa kwa haraka.

Taarifa ya Mwanahabari.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending