News
Zaidi ya familia 5,000 zahofia kufurushwa Matuga,Kwale.
Zaidi ya familia elfu 5 eneo la Matuga kaunti ya Kwale zinahofia kufurushwa katika ardhi zao yenye zaidi ya ekari elfu 6.
Ardhi hizo zilikamilisha mda wa malipo ya kodi kwa waekezaji tangu 2011 na kutarajiwa kurejeshewa wakaazi, japo zinadaiwa kuchukuliwa na mabwenyenye katika njia tatanishi.
Wakiongozwa na mwenyekiti wao Mwafitina Juma Bakari wakaazi hao walisema kwamba licha ya tume ya ardhi nchini NLC kuzuru katika ardhi hizo mapema mwaka 2025, hadi sasa hakuna chochote kinachofanyika.
“Block ten kwanza walikuwa wanasema nyumba ni tatu wale mabwenyenye katika historia ambayo iko pale, lakini walipokuja NLC wakazunguka wakaona nyumba zaidi ya 300 wakashanga, halafu block hiyo hiyo tulikuwa tumeandikiwa barua na NCL mwaka 2011 kwamba tupimiwe na tuko na barua, lakini twashangaa mpaka sasa twashangaa haijapimwa na bwenyenye amerejea na kuchukua shamba”, walisema wakaazi.
Wakaazi hao walimtaka Rais Ruto kuingilia kati mzozo huo ili kuhakikisha jamii hizo zinapata haki.
Vile vile walieleza mahangaiko yao na kuashiria kuchoshwa na dhulma za kihistoria za ardhi.
“Watu wapwani tunadhulumika, watu wa Kwale tunadhulumika, watu wa Waa Ng’ombeni tunadhulumika, tunaomba aingilie kati kwa sababu hata hiyo mambo ya blue economy hatuna nafasi nayo kwa sababu mashamba bwenyenye anapima mpaka baharini, sasa hatua sehemu za kuegesha maboti, hatuna lolote”,waliongeza wakaazi.
Waliishikilia kuwa iwapo suala hilo halitaangaziwa huenda wakalazimika kuandamana hadi ofisi kuu za tume ya ardhi NLC jijini Nairobi kudai haki zao.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

