News
Utata wa uongozi wakumba kanisa la Wesley, Mombasa
Waumini wa kanisa la Wesley Methodist kaunti ya Mombasa wametoa wito kwa usimamizi wa kanisa hilo kutafuta suluhu la kudumu kutokana na mvutano ambao umekuwa ukishuhudiwa mara kwa mara kuhusu uongozi.
Siku ya Jumapili 27, Julai 2025 kulishuhudiwa mvutano kwenye makao makuu ya kanisa hilo baada ya baadhi ya waumini kuzuiliwa kuingia katika kanisa hilo kushiriki ibada ya jumapili.
Kulingana na baadhi ya maaskofu wa kanisa hilo, waumini hao walizuiliwa kuingia katika kanisa hilo baada ya kupinga uteuzi wa askofu mpya Stephen Kanyaru.
Kwenye kikao na waandishi wa habari askofu David Ochami alikashifu kitendo hicho na kusema ni lazima kuwe na usawa kwa kila mmoja katika nyumba za ibada.
“Tunaenda mahali ya kwamba nyumba ya Mungu itakuwa ni ya watu flani jambo ambalo ni kinyume cha neno la Mungu, ya kwamba nyumba ya Mungu ni ya wote, tajiri, masikini, kabila zote maana sote tumetengenezwa kwenye mfano wa Mungu’’, alisema askofu Ochami
Naye askofu Robert Mboya alisema kuwa uteuzi wa askofu Kanyaru haukutekelezwa kwa usawa na watahakikisha aliyepokonywa nafasi hiyo anarejeshwa uongozini.
Taarifa ya Janet Mumbi.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

