Connect with us

News

Ziara ya Rais Ruto Pwani yasheheni ahadi nono

Published

on

Zaira ya rais William Ruto ya siku tano katika ukanda wa Pwani imeonekana kuwa na ahadi nono kwa wenyeji huku zaidi ya takribani shilingi bilioni 85 zikitengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo

Rais Ruto akiwa katika kaunti ya Mombasa, aliahidi utoaji wa hatimiliki za ardhi laki mbili kwa wenyeji, akisema suala hilo litatekelezwa baada ya mazungumzo na baadhi ya wamiliki wa ardhi wasiokupo.

Wakati wa halfa hiyo ya Mombasa, rais Ruto aliwakabidhi wakaazi wa Pwani zaidi ya hatimiliki za ardhi elfu 33 na kuahidi ugavi wa hatimiliki zengine za ardhi laki mbili.

Suala la mpango wa uchumi sawamati, rais aliahidi kima cha shilingi bilioni 10 huku shilingi bilioni 50 zikielekezwa kwa mradi wa dongo kundu.

Ujenzi wa gorofa ya 16 ya nyumba za bei nafuu kaunti ya Mombasa

Katika kaunti ya Kilifi, ziara ya rais haikuwa tu ziara ya uzinduzi wa miradi ya maendeleo bali pia ilisheheni ahadi ya shilingi bilioni 18.

Ambapo fedha hizo zimetengewa miradi mbalimbali ikiwemo shilingi bilioni 7 za ujenzi wa barabara hasa barabara ya kilimita 35 kutoka Tezo-Kakanjuni-Jaribuni hadi Ganze kwa shilingi bilioni 2.2, shilingi bilioni 12 zikitengewa usambazaji wa umeme huku shilingi bilioni 22 kufanikisha ujenzi wa nyumba za bei nafuu.

Mradi wa ujenzi wa nyuma za wafanunzi kwenye vyuo vikuu, vyuo vya kiufundi, na KMTC ukitengewa shilingi bilioni 2 huku ahadi ya hatimiliki elfu 200 ikiendelea kutolewa na rais kwa wenyeji.

Ziara ya rais Ruto katika kaunti ya Kwale ilisheheni pia ahadi ya mabilioni ya pesa, ujenzi wa nyumba za bei nafuu wa shilingi bilioni 15, shilingi bilioni 2 kwa mradi wa ujenzi wa bandari ya Shimoni, huku shilingi bilioni 1.8 kwa usambazaji wa umme miongoni mwa miradi mingine.

Mikakati ya usambazaji umme kwa umma wazinduliwa rasmi na Rais Ruto

Kaunti ya Lamu na Tanariver pia hazikiachwa nyuma katika ziara ya rais ambapo bandari ya Lamu ikimulikwa kwa upanuzi zaidi ili kufungua ajira kwa vijana sawa na ujenzi wa masoko huku soko la Mpeketoni ikitengewa shilingi milioni 290 huku shilingi milioni 315 kufanikisha ujenzi wa Ua kwenye hifadhi ya Tsavo sawa na kufutilia mbali uhifadhi ya Shirango katika wadi ya Bamba ili kuzuia mizozo ya wanyamapori.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mbunge wa Nyali amepuzilia mbali madai ya kuhusishwa na siasa za ukabila

Published

on

By

Mbunge wa Nyali kaunti ya Mombasa Mohamed Ali amepuzilia mbali madai ya kuhusishwa na siasa za ukabila kwenye kaunti hiyo, akisema anafanya siasa zake bila kujali dini, kabila au hata eneo.

Akizungumza huko Nyali, Ali alisema kuna baadhi ya viongozi katika kaunti ya Mombasa, ambao wamekuwa wakiendekeza propaganda za kumhusisha na siasa za migawanyiko ili kumharibia jina taifa linapojiandaa kwa uchaguzi mkuu ujao wa 2027.

Ali ambaye alitangaza kuwania wadhifa wa ugavana kaunti ya Mombasa, aliwataka viongozi kufanya siasa zao kwa kunadi sera zao kwa wakaazi na maendeleo ambayo watatekeleza na sio kutumia suala la ukabila kuwachafulia wengine jina.

“2017 hakuna mtu aliniita mkabila, 2022 hakuna mtu aliniita mkabila, 2027 wanasema Mohamed Ali ni mkabila.Mimi Mohamed Ali, mimi nauliza nikisimama hapa juu ya gari, niseme kabila zote za Kenya wanaweza pewa nafasi ya ugavana ni kuna makosa?,basi sasa wanazunguka wakisema Mohamed ni mkabila kwasababu ameanza kufungua watu macho’’ alisema Ali.

Aidha, Ali alisema ataendelea kuzuru maeneo mbalimbali ya kauti ya Mombasa kunadi sera zake na kuwataka wakaazi wa kaunti hiyo kuwachagua viongozi wanaofaa ambao wataimarisha kaunti hiyo kimaendeleo.

‘’Mimi nimewaambia nitatembea hii Mombasa kwa uwezo wake mwenyezi mungu kutetea wananchi wa Mombasa’’ aliongeza Ali

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Wakimbizi nusu milioni wakabiliwa na baa la njaa, Dadaab

Published

on

Ripoti iliyotolewa hivi karibu na Shirika la Chakula duniani WFP ilionyesha kwamba zaidi ya wakimbizi nusu milioni wanaoishi katika kambi za wakimbizi za Kakuma na Dadaab zilizoko nchini Kenya, wako katika hatari ya kuangamia kutokana na baa la njaa.

Kambi hizi ambazo zinahifadhi wakimbizi wengi zaidi kutoka nchini Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Somalia, ziko hatari iwapo zitakosa misaada ya chakula.

Kufuatia hali hiyo ambayo pia imechangiwa na mashirika ya kimataifa kusitisha ufadhili, sasa hali huenda ikawa tofauti baada ya taifa la Korea kwa ushirikiano na Kenya kutoa ufadhili wa shehena ya nafaka ya zaidi ya tani elfu 10 ambayo inakadiriwa kuwa kima cha shilingi milioni 1.2.

Katibu katika Idara ya uhamiaji nchini Belio Kipsang, aliyepokea msaada huo wa Chakula mjini Mombasa na kuhifadhiwa katika maghala ya Shirika la WFP, ameonya kwamba iwapo Kenya itakosa kupokea msaada kutoka kwa washirika na wafadhili wengine, basi italazimika kuchukua maamuzi magumu, ikiwemo kuwaondoa baadhi ya wakimbizi.

“Nyuma ya kila takwimu kuna familia ambazo ustahimilivu wao unaendelea kujaribiwa kila siku: akina mama wanaokosa kula ili watoto wao wapate chakula, watu walio katika mazingira hatarishi wakiruka milo, na vijana wanaokabiliwa na mustakabali usio na uhakika. Hizi si takwimu za kufikirika. Zinawakilisha watu halisi ambao heshima yao, afya yao na matarajio yao ya maisha yanategemea maamuzi tunayofanya kwa pamoja,” alisema.

Wakati wa hafla hiyo ya kupokea msaada huo wa chakula kwa wakimbizi wa Kakuma na Dadaab, Mkurugenzi wa Shirika la WFP nchini Kenya Betty Ka, alisema shehena ya nafaka itasaidia kuwahudumia takribani wakimbizi nusu milioni katika miezi ijayo.

“Usafirishaji huu unaonyesha umuhimu wa ushirikiano imara katika mnyororo wa ugavi wa misaada ya kibinadamu, ambapo ushirikiano huu kati ya Kenya, Mamlaka ya bandari Kenya (KPA), Shirika la viwango la Kenya(KEBS) na mpango wa Chakula Duniani (WFP) kwa kuhakikisha kwamba chakula cha msaada kinafanikishwa”,alisema Betty.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending