Connect with us

News

Wadau wa sekta ya uchukuzi wasitisha mgomo wao

Published

on

Maafisa wa sekta ya uchukuzi wameahirisha mgomo wao baada ya mazungumzo yaliyoongozwa na Rais William Ruto katika ikulu ya Mombasa.

Maafisa hao wakiongozwa na rais wa Muungano wa wamiliki wa matatu Albert Karagacha wamesema kuwa mengi ya masuala waliokuwa nayo ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta nchini yameangaziwa kwa kina na rais Ruto.

Karagacha amewataka wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa umma pamoja na wamiliki wa magari ya uchukuzi wa mizigo kuhakikisha wanarudisha magari yao barabarani, akisema masuala waliowasilisha kwa rais yameangaziwa

Akizungumza mda mfupi baada ya kufanya kikao na rais William Ruto mjini Mombasa, Karagacha amesema serikali imekuwa kiangazia kwa kina masuala mbali mbali yanayohusu sekta ya uchukuzi nchini.

Aidha amesema iwapo bado serikali itakuwa inajikokota katika kufanikisha masuala waliojadiliana basi wataitisha mazungumzo zaidi na Wizara husika ili kuafikiwa kwa ajenda zao huku akisema japo suala la mzozo wa mafuta sio jambo la Kenya pekee lakini taifa inawajibu wa kusaidia wananchi wake.

Wakati huo huo Karagacha amewataka wakenya kutoingiza siasa katika suala la kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mshukiwa wa ulanguzi na usafirishaji wa watoto anyimwa dhamana

Published

on

By

Mahakama ya Shanzu imemnyima dhamana mshukiwa wa ulanguzi wa watoto zaidi ya 20.

Mahakama imeagiza mshukiwa huyo kuzuiliwa rumande ili kuwawezesha maafisa wa polisi kukamilisha uchunguzi wao.

Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa huyo Almasi Rama Amos mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa na maafisa wa upelelezi kutoka kitengo cha kupambana na ulanguzi wa binadamu na ulinzi wa watoto (AHTCPU) pamoja na maafisa wa idara ya upelelezi wa Jinai kutoka kaunti ya Mombasa.

Kukamatwa kwake kufuatia wiki kadhaa za uchunguzi kuhusu ripoti za unyanyasaji wa watoto zinazowalenga wasichana wadogo walio katika mazingira magumu.

Rama, anayetuhumiwa kwa kujihusisha na kundi linalodaiwa kuwa la ulanguzi wa watoto na dhulma za kingono na kufikishwa katika Mahakama ya Shanzu kufuatia operesheni ya kiusalama iliyoidhinishwa na maafisa hao.

Rama alipatikana katika mtaa wa Nguu Tatu eneo la Concordia katika kaunti ndogo ya Kisauni akiwa na watoto watatu wa kike.

Mahakama imeelezwa kuwa mshukiwa anadaiwa kuendesha “vituo vya uokoaji” katika kaunti za Mombasa na Kilifi kwa kujifanya kuwalea na kuwapa ushauri.

Kulingana na uchunguzi vituo hivyo vilikuwa vikitumika kama msingi wa dhulma za kingono na unyanyasaji wa watoto.

Alipokamatwa, mshukiwa aliwaongoza maafisa hadi kituo chengeni eneo la Ribe katika eneo bunge la Rabai, ambapo maafisa wa upelelezi waliwaokoa watoto 19 wa jinsia ya kike na kufikisha jumla ya waathiriwa waliookolewa kufikia ishirini na wawili (22).

Mbele ya Mahakama ya Shanzu tarehe 21 Mei, 2026, mshukiwa amekabiliwa na mfululizo wa mashtaka, ikiwemo unajisi, biashara ya watoto kwa madhumuni ya kuwadhulumu kingono pamoja na unyanyasaji wa watoto ambapo amekana mashtaka hayo.

 Kesi hiyo imepangwa kutajwa Juni 8, 2026.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Vijana na akina mama hawashiriki vikao vya ukusanyaji maoni Kilifi

Published

on

By

Imebainika kuwa idadi kubwa ya wanawake na vijana katika kaunti ya Kilifi bado hawajahamasishwa vilivyo kuhusiana na masuala ya uongozi, uundaji wa bajeti na sera katika serikali za kaunti na serikali kuu.

Katika kikao cha uzinduzi wa mradi wa meaningful Engagement And Transformative Action ( META) ambacho kimeandaliwa na Shirika la Timiza Youth Initiative na kuwaleta pamoja wadau mbalimbali, viongozi wa kaunti ya Kilifi, waandishi wa habari, vijana na akina mama.

Kulingana na Mwenyekiti wa Shirika la Timiza Youth Initiative Brian Mundia, hatua ya kuwatenga vijana na akina mama pamoja na wadau mbalimbali katika kutoa maoni yao kuhusu miradi ya maendeleo kumechagia wengi wao kusalia nyuma katika masuala yanayohusu maendeleo, uongozi na matumizi ya mitandao.

Mundia alisema mradi huo ambao pia unawalenga watu walio na uatilifu, wanapania kuzuru hadi maeneo ya mashinani kuhakikisha kuna hamasa ya kutosha na namna ya kutumia mitandao ya kidijitali kujibunia nafasi za ajira na wanashirikiana na wizara ya jinsia ile ya ugatuzi na mazingira kaunti ya Kilifi ili kufanikisha suala hilo.

Kwa upande wake Jackline Waweru wa shirika la Leadership For Impact, alisisitiza umuhimu wa vijana na akina mama kuhamasishwa kuhusu umuhimu wa kushiriki upigaji wa kura ili kuwaepusha kutumiwa visivyo na wanasiasa.

Ni kauli ambazo ziliungwa mkono na Waziri wa ugatuzi kaunti ya Kilifi, Clara Chonga ambaye alisema wanaweka mikakati kuhakikisha Wananchi wa kaunti ya Kilifi wanaweza kushiriki zoezi la ukusanyaji wa maoni pia kupitia mfumo wa kidigitali.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending