Connect with us

News

Askofu Kivuva atoa wito kwa serikali kusuluhisha mgomo wa Wahadhiri

Published

on

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mombasa Martin Kivuva ametoa wito kwa serikali pamoja na Wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma nchini kuanzisha mazungumzo ya haraka ili kutatua mgomo wa wahdhiri unaoendelea kote nchini.

Askofu Kivuva alisema mgomo huo ambao sasa umeingia siku ya 11, umeathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma nchini.

Kivuva alisema hali hiyo ikiendelea huenda ikaleta madhara makubwa kwa elimu ya juu na mstakabali wa wanafunzi huku akisisitiza kwamba suluhu la kudumu linaweza kupatikana kupitia mazungumzo ya wazi kati ya pande zote mbili.

“Mgomo sharti uishie watu kuzungumza na kuweka mikakati, siku zote bila maridhiano ama kuridhika moyoni ni vigumu sana watu kusonga mbele, jambo hilo la Wahadhiri kugoma pia ni changamoto inayokumba nyanja ya elimu”, alisema Askofu Kivuva.

Wakati huo huo aliisihi serikali kutimiza ahadi ilizotoa kwa Wahadhiri, ikiwemo kuwalipa mishahara na marupurupu yao, akisisitiza kwamba haki za wafanyakazi ni lazima ziheshimiwe ili kuhakikisha utulivu katika sekta ya elimu.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending