Connect with us

News

Bitok: Serikali kusambaza fedha za shule wiki hii

Published

on

Serikali imetangaza kwamba Fedha za usimamizi wa shughuli za masomo katika shule za umma kote nchini zitasambazwa kabla ya wiki hii kukamilika ili kuwawezesha wanafunzi kuendelea na masomo yao.

Katibu katika Wizara ya Elimu nchini Julius Bitok alisema zaidi ya shule elfu 45 za umma kote nchini zitapokea mgao wa fedha ili kufanikisha shughuli za masomo, akisisitiza kwamba hatua hiyo itadhibiti changamoto za elimu.

Akizungumza na Wanahabari jijini Nairobi, Bitok alisema Wizara ya Elimu nchini ilifanya mazungumzo na Maafisa wa Hazina kuu ya fedha ikiwemo Waziri wa Fedha nchini John Mbadi na kuafikiana kusambazwa kwa shilingi bilioni 23.

“Tumehusisha hazina kuu ya kitaifa ya fedha na pia tumefanya mazungumzo maafisa wa hazina hiyo wakiongozwa na Waziri mwenyewe na tunataka kuwahakikisha wakenya kwamba tumeweka mikakati mwafaka na fedha za usimamizi wa shughuli za masomo zitasambazwa kwa shule elfu 45 kote nchini kabla ya kukamilika kwa wiki hii”, alisema Bitok.

Wakati huo huo, Bitok aliwarai walimu wakuu kote nchini kuhakikisha wanakumbatia kikamilifu mfumo mpya wa elimu nchini CBC, akisema tayari serikali imejitolea kuhakikisha inafanikisha mchakato mzima wa elimu nchini.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending