News
Mung’aro achaguliwa kuwa Mwenyekiti wa ODM kaunti ya Kilifi
Uchaguzi wa viongozi wa mashinani wa Chama cha ODM katika kaunti ya Kilifi ulifanyika Agosti 25, 2025 licha ya awali kuhushudiwa vurugu baada ya kutofautiana kwa wafausi wa chama hicho.
Gavana wa kaunt ya Kilifi Gedion Mung’aro alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi na kuchakuwa nafasi ya Teddy Mwambire, baada ya kumbaduliwa uongozini kama Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi.
Naibu Mwenyekiti wa chama hicho kaunti ya Kilifi alichaguliwa Joseph Chilumo, Katibu mkuu akichaguliwa Ken Chonga ambaye ni mbunge wa Kilifi Kusini na Mwekahazina akachaguliwa Paul Katana ambaye ni Mbunge wa Kaloleni katika uchaguzi huo wa viongozi wa mashinani wa chama cha ODM katika kaunti ya Kilifi.
Mengine waliochaguliwa ni pamoja na Tima Abuu, Abdallah Kombe, Caro Kalume, Mae Mwadena, Nickson Muramba, Harrison Kombe Twahir Abdul, Rashid Mohamed miongoni mwa viongozi wengine.
Vurugu hizo zilitokea wakati wasimamizi kwenye lango la ukumbi huo wanaoegemea mrengo wa Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro, walipodai kwamba baadhi ya wanachama sio wanachama halisi.
Wafuasi wa Mwakilishi wadi ya Ganda Oscar Wanje ambaye alikuwa anawania wadhifa wa uenyekiti wa vijana kaunti ya Kilifi alilazimika kujiondoa katika wadhfa huo kwani ni kati ya miongoni mwa wale waliozuiliwa kuingia katika ukumbi wa uchaguzi huo na nafasi hiyo ikachaguliwa Abdallah Kombe.
Wafuasi hao walikosoa utaratibu mzima wa maandalizi ya uchaguzi huo, wakishikilia kwamba watawasilisha malalamishi yao kwa kamati kuu ya uchaguzi ya chama cha ODM kupinga uchaguzi huo.
Wafuasi hao wakiongozwa na Mwakilishi wadi ya Ganze Karisa Ngirani, walilaumu utaratibu wa shughuli hiyo, wakisema umekosa kuzingatia haki ya wanachama.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

