Connect with us

News

Bunge la seneti kujadili hoja ya kutimuliwa kwa Gavana Mutai

Published

on

Bunge la seneti limetangaza kwamba siku ya Jumatano Agosti 20, 2025 litakuwa na kikao maalum cha bunge ili kujadili hoja mbili muhimu kwa kuambatana na sera za bunge.

Katika notisi ya gazeti rasmi la serikali, kikao cha kwanza itakuwa shughuli ya kuapishwa kwa Seneta mteule Consolata Nabwire ili kuchunua nafasi ya aliyekuwa seneta mteule Gloria Orwoba aliyetimuliwa mamlakani.

Kikao cha pili kitakuwa cha kujadili hoja ya kubanduliwa mamlakani kwa Gavana wa Kericho Dkt Eric Kipkoech Mutai, kikao ambacho kimeratibiwa kuanza rasmi mwendo wa saa nane alasiri.

Gavana Mutai, anakabiliwa na shutma za ufisadi, utumizi mbaya wa raslimali za umma, ukiukaji wa Katiba pamoja na kujinufaisha binafsi na miradi ya umma. 

Maseneta hao hata hivyo baada ya kujadili hoja hiyo na kusikiza pande zote mbili, bunge la seneti litaamua kumnusuru Gavana Mutai ama kumtimua mamlakani. 

Tayari Kenya ina magavana watatu waliotimuliwa uongozi kupitia kura ya kutokuwa na Imani nao baada ya Wawakilishi wadi kutofautiana na magavana wao huku wengine wakipatikana na sakata za ufisadi na ukiukaji wa katiba.

Iwapo Gavana Mutai atatimuliwa mamlakani basi atakuwa anaongeza idadi ya magavana waliotemwa na Wawakilishi wadi kufikia Magavana wanne, akiwemo aliyekuwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu, aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Mbuvi Sonko, aliyekuwa Gavana wa Embu Kawira Mwangaza na Gavana Mutai iwapo hatapokea shoka la kutimuliwa uongozini.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending